• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

DC Kilosa awaasa watendaji wa Kata na Vijiji

Posted on: February 10th, 2022

Watendaji wa kata na vijiji wametakiwa kuridhika na kipato wanachokipata kutokana na majukumu yao  badala kujihusisha na ukusanyaji wa kipato kisicho halali kupitia makusanyo ya fedha za Serikali kwani Serikali imewaamini na kuwaweka ili waweze kuwahudumia wananchi katika maeneo yao lakini pia kufanya kazi kwa kuheshimiana na kuzingatia nidhamu ya kiutendaji kazi.

Wito huo umetolewa Februari 09/02/2022 na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Alhaj Majid Mwanga wakati wa kikao kazi cha Maafisa tarafa, Watendaji wa kata na Vijiji ambapo amewataka kutambua kuwa wao ni watumishi wa umma ambao Serikali imewaamini hivyo wanapaswa kufuata sheria, taratibu na kanuni kadri zinavyowaelekeza katika utendaji wao wa kuwahudumia wananchi.

Mwanga amesema wapo baadhi ya watendaji wanaofanya kazi bila kuzingatia taratibu za kazi ikiwemo kukiuka usimamizi wa mapato kama inavyostahiki  huku akitoa onyo kwa watendaji ambao wamekuwa wakitumia vibaya madaraka yao badala ya kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia taaluma yao vizuri.

Aidha ametaka kila mtendaji kuweka malengo ya ukusanyaji mapato kwa kila katika eneo lake kwa kuzingatia vyanzo vyote vya mapato vilivyopo katika maeneo yao huku akisisitiza kufanyika kwa  zoezi la usafi kila mwisho wa mwezi zoezi ambalo linapaswa kufanyika na watu wote ambapo upande wa mapato amewataka kutambua kuwa moja ya vipimo vinavyotazamwa katika utendaji wao ni ukusanyaji wa mapato ambao kwa sasa umekuwa dhaifu jambo linalopelekea Halmashauri kukusanya kiwango kidogo ilihali mapato yapo ya kutosha ila usimamizi umelegalega.

Pamoja na hayo amesisitiza watendaji hao kutambua kuwa mashine za kukusanyia mapato(POS) ni mali isiyohamishika na kwamba fedha yoyote inayokusanywa kutokana  na vyanzo mbalimbali ipelekwe benki mara moja huku akiagiza vizuizi vyote viimarishwe sambamba  na kuweka usimamizi mzuri wa magulio yote lakini pia ametaka watendaji hao kuendelea kusisitiza wananchi kushiriki zoezi la sensa ya watu na makazi ifikapo mwezi Agosti 2022 sambamba na kuhamasisha wananchi waweze kupata chanjo ya Uviko-19.

Kwa upande wake Katibu Tawala Wilaya Yohana Kasitila amewataka watendaji hao kubadilika katika utendaji wa kazi zao hususani katika suala la ukusanyaji mapato kwa kujiepusha namna yoyote ovu na kuepuka rushwa kwani Serikali iko macho hivyo ni vema wakazingatia zaidi sheria, taratibu na kanuni za kazi lakini pia amewakumbusha kuzingatia uandishi wa barua za kiofisi kwa kufuata ngazi za kimadaraka na kimamlaka pamoja na uvaaji unaozingatia maadili kwa watumishi wa umma.


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa