Mkuu Wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka amewataka vingozi kuanzia ngazi ya Wilaya, Kata na Vijiji kusimamia miradi ipasavyo ili kurekebisha na kutatua kwa haraka changamoto zinazojitokeza lengo likiwa ni kukamilisha miradi kwa wakati na kwa viwango vinavyostahili.
Mhe. Shaka ameeleza hayo Juni 19, 2025 katika ziara yake ya Kukagua miradi mbalimbali ya Maendeleo ambapo amesema viongozi wawajibike ipasavyo katika kutekeleza majukumu yao hususani katika usimamizi mzuri na ufatiliaji wa karibu wa miradi hiyo ili ikamilike kwa wakati na ianze kutoa huduma bora kwa wananchi.
“ Viongozi simamieni miradi kwa karibu, rekebisheni mapungufu au changamoto zinajitokeza na kuhakikisha zinatatuliwa kwa wakati” Alisisitiza Mhe. Shaka
Pia Mhe. Shaka amesihi wasimamizi wa miradi ngazi ya Kata na kijiji kuhamasisha wananchi kujitolea nguvu kazi katika utekelezaji wa miradi hiyo kwa ajili ya maendeleo ya vijiji na Kata.
Ziara hiyo ya siku mbili imehitimishwa leo kwa kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Ujenzi wa shule Mpya ya Sekondari Amali, Ujenzi wa kituo cha Zahanati Kwambe, Ujenzi wa shule mpya ya msingi Matongolo na Ujenzi wa mabweni 2 , madarasa 4 na matundu 10 ya vyoo katika shule ya sekondari Dumila.
Halmashauri ya Wilaya Kilosa
Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa
Simu: 023 2623093
Simu: 0737847880
Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz
Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa