• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

DC SHAKA AWATAKA WAZAZI / WALEZI KUWAJIBIKA KATIKA MALEZI BORA YA WATOTO

Posted on: June 16th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka amewataka Wazazi , walezi, viongozi wa dini na wadau mbalimbali wa maendeleo kukumbuka jukumu  lao la kuwalinda watoto ili kuwajengea ustawi wa kesho kwa kuwaunda kuwa watumishi bora katika Taifa la kesho.


Mhe. Shaka ameyasema hayo Juni 16, 2025 akimwakilisha Mkuu wa Mkoa Wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika kimkoa Wilayani Kilosa katika Viwanja vya Shule ya Msingi Kilosa Town ambapo amesema wazazi wanatakiwa kukaa karibu na watoto ili kujua wanayoyapitia na wawe huru kutoa taarifa pindi wanapofanyiwa vitendo viovu.

Sambamba  na hayo amewataka  Maafisa   Maendeleo  na Ustawi wa jamii katika ngazi ya Halmashauri  na Kata waendelee kuimarisha elimu, malezi na makuzi ya watoto kwa wazazi na walezi ili waelewe wajibu wao wa kuwalea watoto kwa kuzingatia misingi  ya haki na usawa wa kijinsia.

Aidha Shaka ameongeza kwa kusema kuna ripoti mbalimbali zimeeleza kuwa  bado  watoto  wanakabiliwa na changamoto za vitendo vya ukatili wa aina mbalimbali  ikiwemo ubakaji, ulawiti, utumikishwaji  katika ajira hatarishi, utekaji, vipigo, kuchomwa moto, mimba za utotoni na ukatili wa mitandaoni ambapo  katika kuhakikisha haki za watoto zinalindwa serikali kwa kushirikiana na wadau imefanya  jitihada za kuratibu na kusimamia program ya taifa ya malezi, makuzi na maendeleo ya mtoto kwa mwaka 2020/ 2025.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii  Mkoa wa Morogoro  Gibson  Mwakoba amesema maadhimisho hayo yametokana  na tukio la Mauaji  ya watoto elfu mbili ambalo   lilitokea  Juni  16, 1976 katika  Kitongoji cha Soweto  Nchini  Afrika Kusini  ambapo mauaji hayo yalitokea baada ya watoto hao kuamua kuandamana  kudai haki  yao ya kutobaguliwa sawasawa na wengine hivyo  Jamii  na wazazi  wote wanapaswa kuhakikisha  kuwalinda Watoto  dhidi ya vitendo vya ukatili.

Maadhimisho  hayo  yamehudhuriwa  na Viongozi mbalimbali ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata Wadau mbalimbali wa maendeleo, watoto na wananchi kwa ujumla yakiambatana na kauli mbiu isemayo “HAKI ZA MTOTO ,TULIPOTOKA ,TULIPO NA TUENDAKO”

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI KILOSA DC June 06, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • DC SHAKA AWATAKA VIONGOZI NGAZI YA KATA NA VIJIJI KUSIMAMIA NA KUFUATILIA MIRADI YA MAENDELEO IPASAVYO

    June 19, 2025
  • DC SHAKA AWATAKA WAZAZI / WALEZI KUWAJIBIKA KATIKA MALEZI BORA YA WATOTO

    June 16, 2025
  • TIMU YA MENEJIMENTI KILOSA YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    June 12, 2025
  • RC MALIMA ATOA MAAGIZO KILOSA, AITAKA HALMASHAURI KUBORESHA UKUSANYAJI WA MAPATO

    June 11, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa