• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Halmashauri ongezeni nguvu katika sekta ya kilimo - DC Mgoyi

Posted on: March 10th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ametoa rai kwa Halmashauri ya Wilaya ya  Kilosa kutambua kuwa Wilaya ya Kilosa ni wilaya ya kilimo iliyojaa mito yenye maji ya kutosha hivyo ni vema wilaya ikajikita zaidi katika uzalishaji ili kupata mazao ambayo yatapelekwa kiwandani huku akitaka Halmashauri kupanga bajeti ya kutosha upande wa kilimo na kuwekeza zaidi katika kilimo ili kupata tija zaidi.

Mgoyi amesema kwa sasa wilaya imekuwa ikipanda kiwango cha uzalishaji hali inayoonyesha kuongezeka kwa maeneo ya kulima huku migogoro ya wakulima na wafugaji ikipungua na kupelekea wananchi kuweza kulima na kuvuna huku akisema kuwa wakulima wanahitaji zaidi huduma za ugani kwa kuhakikisha huduma hizo zinapatikana ili kuzalisha kiwango kinachotarajjiwa .

Pamoja na hayo amesisitiza kuwepo kwa mashamba darasa ya kijiji kwa kila kijiji kwani mashamba hayo yatasaidia wananchi kujifunza namna ya kilimo bora halikadhalika namna ya kuhifadhi mazao yao baada ya kuvuna kwani kumekuwa na changamoto kubwa ya kuhifadhi mazao ambayo kwa asilimia kubwa mengi yamekuwa yakitunzwa katika namna isiyo sahihi na kupelekea upotevu wa mazao sambamba upatikanaji wa vifaa vya kuhifadhia mazao.

Aidha ametoa wito kwa MVIWATA licha ya kufanya mambo mazuri amewata kuunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya tano kwa kuwa na semina nyingi zaidi kwa wakulima lengo ikiwa ni kuwasaidia wakulima katika kuongeza ujuzi na hamasa kwa wakulima ili waweze kupiga hatua zaidi na kukuza uchumi wao kwani wanahitaji zaidi kujengewa uwezo na kwamba Serikali iliyopo madaraka imejikita zaidi katika kutetea wanyonge. 

Naye Mratibu wa MVIWATA Morogoro Joseph Sengasenga amesema MVIWATA inashirikiana na Halmashauri kwa kufanya mafunzo mbalimbali ikiwemo mafunzo ya ujasiriamali wa aina mbalimbali, kuzalisha kwa tija lakini pia ina mpango wa kuanzisha mashamba darasa kwa ajili ya wakulima ili waweze kujifunza zaidi na kwamba inatekeleza shughuli zake kwa kushirikiana na Halmashauri kwani wanufaika wa shughuli mbalimbali zinazofanywa  ni kwa faida ya wakulima na wananchi kiujumla.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUKODISHA MASHAMBA YA HALMASHAURI September 11, 2025
  • TANGAZO LA TOZO September 10, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI KILOSA DC June 06, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA November 23, 2023
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • SERIKALI YASHIRIKIANA NA CAMFED KUFIKISHA HUDUMA YA MAJI SHULE ZA MSINGI KILOSA

    September 03, 2025
  • WAZAZ/WALEZI WAHIMIZWA KUCHANGIA CHAKULA SHULENI ILI KUONGEZA UFAULU NA KUPUNGUZA UTORO

    September 03, 2025
  • KILOSA YATOA MILIONI 541.3 MIKOPO YA 10 % KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

    August 27, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KWA KASI KATIKA JIMBO LA KILOSA NA MIKUMI

    August 21, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa