• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Halmashauri ongezeni nguvu katika sekta ya kilimo - DC Mgoyi

Posted on: March 10th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ametoa rai kwa Halmashauri ya Wilaya ya  Kilosa kutambua kuwa Wilaya ya Kilosa ni wilaya ya kilimo iliyojaa mito yenye maji ya kutosha hivyo ni vema wilaya ikajikita zaidi katika uzalishaji ili kupata mazao ambayo yatapelekwa kiwandani huku akitaka Halmashauri kupanga bajeti ya kutosha upande wa kilimo na kuwekeza zaidi katika kilimo ili kupata tija zaidi.

Mgoyi amesema kwa sasa wilaya imekuwa ikipanda kiwango cha uzalishaji hali inayoonyesha kuongezeka kwa maeneo ya kulima huku migogoro ya wakulima na wafugaji ikipungua na kupelekea wananchi kuweza kulima na kuvuna huku akisema kuwa wakulima wanahitaji zaidi huduma za ugani kwa kuhakikisha huduma hizo zinapatikana ili kuzalisha kiwango kinachotarajjiwa .

Pamoja na hayo amesisitiza kuwepo kwa mashamba darasa ya kijiji kwa kila kijiji kwani mashamba hayo yatasaidia wananchi kujifunza namna ya kilimo bora halikadhalika namna ya kuhifadhi mazao yao baada ya kuvuna kwani kumekuwa na changamoto kubwa ya kuhifadhi mazao ambayo kwa asilimia kubwa mengi yamekuwa yakitunzwa katika namna isiyo sahihi na kupelekea upotevu wa mazao sambamba upatikanaji wa vifaa vya kuhifadhia mazao.

Aidha ametoa wito kwa MVIWATA licha ya kufanya mambo mazuri amewata kuunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya tano kwa kuwa na semina nyingi zaidi kwa wakulima lengo ikiwa ni kuwasaidia wakulima katika kuongeza ujuzi na hamasa kwa wakulima ili waweze kupiga hatua zaidi na kukuza uchumi wao kwani wanahitaji zaidi kujengewa uwezo na kwamba Serikali iliyopo madaraka imejikita zaidi katika kutetea wanyonge. 

Naye Mratibu wa MVIWATA Morogoro Joseph Sengasenga amesema MVIWATA inashirikiana na Halmashauri kwa kufanya mafunzo mbalimbali ikiwemo mafunzo ya ujasiriamali wa aina mbalimbali, kuzalisha kwa tija lakini pia ina mpango wa kuanzisha mashamba darasa kwa ajili ya wakulima ili waweze kujifunza zaidi na kwamba inatekeleza shughuli zake kwa kushirikiana na Halmashauri kwani wanufaika wa shughuli mbalimbali zinazofanywa  ni kwa faida ya wakulima na wananchi kiujumla.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Kilosa kufanya sensa ya mifugo

    December 29, 2022
  • Kilosa kunufaika na mradi wa BOOST

    December 24, 2022
  • Kilosa yaendelea kutambua juhudi za Serikali kwa Watumishi wa Umma na Wananchi-DED Kilosa

    December 19, 2022
  • -Serikali haitosita kulinda Rasilimali watu kwa maslahi ya Maendeleo ya Taifa- Mh. Mhagama

    December 20, 2022
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa