Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ikiongonzwa na Makamu Mwenyekiti wake Mhe. Hassan Mkopi leo Mei 20, 2025 imefanya ziara ya kutembelea mradi wa Shule ya Sekondari Masanze iliyopo Kata ya Masanze ambapo ameipongeza Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa (CMT) kwa usimamizi mzuri wa mradi huo.
Akizungumza wakati wa Ziara hiyo Mhe. Mkopi amesema ameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo na kwa kazi nzuri inayoendelea kufanyika hivyo ameutaka uongozi wa shule kutoa ushirikiano hasa wakati changamoto zinapojitokeza ili ziweze kutatuliwa na miradi hiyo kukamilika kwa wakati.
Akisoma taarifa ya Mradi Mkuu wa shule hiyo Mwl. Laurent A.Bundala amesema mradi huo utagharimu kiasi cha shilingi 346,000,000 mpaka kukamilika kwake fedha kutoka serikali kuu kwa ajili ya madarasa 4, mabweni 2, matundu 10 ya vyoo ambapo Mwl. Bundala ameongeza kuwa Madarasa 4 yapo hatua ya ufungaji wa gypsum, Mabweni 2 yapo hatua ya kupiga plaster na Matundu 10 ya vyoo yakiwa hatua ya kumwagaji jamvi.
Halmashauri ya Wilaya Kilosa
Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa
Simu: 023 2623093
Simu: 0737847880
Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz
Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa