Watendaji wa Kata wametakiwa kuacha kusaini vibali vya kuwahuruhusu au kuwakaribisha wafugaji kuingi katika vijiji vingine pasipo kufuata utaratibu na kusababisha migogoro ya wakulima na wafugaji ambapo kwa sasa hakuna maeneo kwa ajili ya malisho ya mifugo.
Hayo yameelezwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Ndg. Elia Shemtoi wakati wa kikao cha Watendaji wa Kata na Menejimenti (CMT) kilichofanyika Mei 28,2025 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo ambapo amewahimiza watendaji hao kuongeza juhudi ya kupunguza migogoro hiyo ambayo ni changamoto kubwa katika Wilaya ya Kilosa.
Pia Elia amewataka watendaji hao kuongeza juhudi ya ukusanyaji wa Mapato kwa kusimamia ipasavyo vyanzo vya mapato ikiwemo kukodisha mashamba ya kijiji ,kutoza kodi za vilabu vya pombe ,masoko pamoja na stendi ili kuweza kapata fedha kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo .
Kwa upande wake Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Morogoro Ndg. Idrisa Kayera ameeleza kuwa changamoto kubwa katika Mkoa mzima wa Morogoro ikiwemo wilaya ya Kilosa ni pamoja na uvamizi ardhi ambao unasabibishwa na baadhi ya viongozi wa umma kuwaruhuhu wafugaji kuingia katika vijijini bila kufuata utaratibu hivyo ni uwajibu wao kuhakikisha wanapuguza migogoro hiyo katika maeneo yao.
Katika kikao hicho waliwapongeza baadhi ya watendaji wa kata waliofanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato ikiwemo Kata ya Magomeni, Kimamba A, Kitete na Mabwerere ikiwa tayari wamevuka lengo katika ukusanyaji mapato.
Halmashauri ya Wilaya Kilosa
Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa
Simu: 023 2623093
Simu: 0737847880
Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz
Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa