• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MH. MASAUNI ATIA NENO JUHUDI ZA SERIKALI

Posted on: February 21st, 2023

Wananchi wametakiwa kutambua jitihada mbalimbali ambazo serikali inazifanya katika kuhakikisha wananchi wanaishi  katika mazingira mazuri ikiwemo katika kuwaletea miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na utatuzi wa changamoto zinazowakabili wananchi na kwamba jambo lolote linalofanywa na wananchi kwa ajili ya maendeleo serikali haitosita kuliunga mkono.

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh, Hamad Masauni alipokuwa akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Mikumi ambapo amesema Serikali imekuwa ikifanya kazi kubwa katika kuendeleza miradi mbalimbali, huku akisema kuwa Serikali ya awamu ya sita imejipanga kwa dhati kuwahakikishia wananchi usalama wao na mali zao kwa kuendelea kujenga vituo vya polisi na nyumba za polisi katika maeneo mbalimbali ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za kiusalama.

Akizungumzia suala la migogoro ya wakulima na wafugaji ambalo pia linahusisha jeshi la polisi katika kuzuia vurugu na migogoro hiyo ametaka kila kiongozi mwenye mamlaka katika eneo lake kuwa sehemu ya utatuzi wa migogoro hiyo huku akitaka polisi kata kuweka juhudi za makusudi katika kutimiza majukumu yao ya kuwahudumia wananchi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu,sambamba kutoa elimu ya ulinzi shirikishi kwa wananchi lakini pia kukemea na kuchukua hatua stahiki kwa wote wanaohusika na kesi mbalimbali za ubakaji ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Aidha amelitaka jeshi la magereza kuwekeza zaidi katika kuendelea kutumia rasilimali walizonazo katika kuisadia Serikali  kutimiza adhma yake ya kuhudumia wananchi kwani jeshi hilo lina wataalam wakutosha ambao wana uwezo wa kusababisha mabadiliko chanya kwa jamii na Serikali kiujumla.

Naye Mbunge wa Jimbo la Mikumu Mh Dennis Londo ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa fedha nyingi ambazo Jimbo la Mikumi limepokea kwa ajili ya miradi ya maendeleo lakini pia amemuomba waziri huyo kuongeza nguvu katika kuiesema miji ambayo inapaswa kupewa hadhi ya kuwa halmashauri kwa lengo la kusaidia upatikanaji wa miradi ya kimkakati huku akiomba kufanyika kwa maboresho ya upatikanaji wa kituo kikubwa cha polisi pamoja na vituo vidogo  kwa baadhi ya maeneo kwani maeneo mengi ya wilaya hayana vituo vidogo vya polisi,uboreshwaji wa njia za mawasiliano huku akishauri kufanyika kwa miundombinu ya barabara kwa kiwango cha lami kutoka Kilosa-Mikumi jambo litakalosaidia wananchi kutotumia umbali mrefu kuelekea maeneo mbalimbali.

Kwa upande wa viongozi wa jeshi la Magereza Mkuu wa gereza mkoa wa Morogoro ACP Dkt. Wilson Rugamba na Mkuu wa gereza Kilosa ASP Dominick Mshana wamesema jeshi la magereza liko tayari kutekeleza na kupokea mabadiliko chanya yanayoendelea ndani ya Serikali na kwamba wanajipanga kuwa na jeshi la kisasa lenye tija kwa ajili ya kuzalisha hususani katika kilimo kwa kutumia rasilimali zilizopo kutokana na ardhi ya kilimo waliyonayo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa