• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MH. MASAUNI ATIA NENO JUHUDI ZA SERIKALI

Posted on: February 21st, 2023

Wananchi wametakiwa kutambua jitihada mbalimbali ambazo serikali inazifanya katika kuhakikisha wananchi wanaishi  katika mazingira mazuri ikiwemo katika kuwaletea miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na utatuzi wa changamoto zinazowakabili wananchi na kwamba jambo lolote linalofanywa na wananchi kwa ajili ya maendeleo serikali haitosita kuliunga mkono.

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh, Hamad Masauni alipokuwa akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Mikumi ambapo amesema Serikali imekuwa ikifanya kazi kubwa katika kuendeleza miradi mbalimbali, huku akisema kuwa Serikali ya awamu ya sita imejipanga kwa dhati kuwahakikishia wananchi usalama wao na mali zao kwa kuendelea kujenga vituo vya polisi na nyumba za polisi katika maeneo mbalimbali ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za kiusalama.

Akizungumzia suala la migogoro ya wakulima na wafugaji ambalo pia linahusisha jeshi la polisi katika kuzuia vurugu na migogoro hiyo ametaka kila kiongozi mwenye mamlaka katika eneo lake kuwa sehemu ya utatuzi wa migogoro hiyo huku akitaka polisi kata kuweka juhudi za makusudi katika kutimiza majukumu yao ya kuwahudumia wananchi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu,sambamba kutoa elimu ya ulinzi shirikishi kwa wananchi lakini pia kukemea na kuchukua hatua stahiki kwa wote wanaohusika na kesi mbalimbali za ubakaji ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Aidha amelitaka jeshi la magereza kuwekeza zaidi katika kuendelea kutumia rasilimali walizonazo katika kuisadia Serikali  kutimiza adhma yake ya kuhudumia wananchi kwani jeshi hilo lina wataalam wakutosha ambao wana uwezo wa kusababisha mabadiliko chanya kwa jamii na Serikali kiujumla.

Naye Mbunge wa Jimbo la Mikumu Mh Dennis Londo ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa fedha nyingi ambazo Jimbo la Mikumi limepokea kwa ajili ya miradi ya maendeleo lakini pia amemuomba waziri huyo kuongeza nguvu katika kuiesema miji ambayo inapaswa kupewa hadhi ya kuwa halmashauri kwa lengo la kusaidia upatikanaji wa miradi ya kimkakati huku akiomba kufanyika kwa maboresho ya upatikanaji wa kituo kikubwa cha polisi pamoja na vituo vidogo  kwa baadhi ya maeneo kwani maeneo mengi ya wilaya hayana vituo vidogo vya polisi,uboreshwaji wa njia za mawasiliano huku akishauri kufanyika kwa miundombinu ya barabara kwa kiwango cha lami kutoka Kilosa-Mikumi jambo litakalosaidia wananchi kutotumia umbali mrefu kuelekea maeneo mbalimbali.

Kwa upande wa viongozi wa jeshi la Magereza Mkuu wa gereza mkoa wa Morogoro ACP Dkt. Wilson Rugamba na Mkuu wa gereza Kilosa ASP Dominick Mshana wamesema jeshi la magereza liko tayari kutekeleza na kupokea mabadiliko chanya yanayoendelea ndani ya Serikali na kwamba wanajipanga kuwa na jeshi la kisasa lenye tija kwa ajili ya kuzalisha hususani katika kilimo kwa kutumia rasilimali zilizopo kutokana na ardhi ya kilimo waliyonayo.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Mfumo wa TAUSI watambulishwa kwa wafanyabiashara

    March 23, 2023
  • Shule ya Msingi Tambukareli yaanza kutumika rasmii

    March 06, 2023
  • Shule ya Msingi Tambykareli yaanza kutumika rasmi

    March 06, 2023
  • DC SHAKA ASISITIZA UONGOZI WA PAMOJA

    March 01, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa