• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

BENKI YA NMB YATOA MSAADA WENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 33.1 WILAYANI KILOSA

Posted on: August 28th, 2024

Katika kuunga mkono juhudi za Serikali kwenye Sekta ya Afya na Elimu benki ya NMB imetoa msaada wa Madawati,Viti, Meza na Vifaa tiba ikiwemo Mashine za kupimia presha,Magodoro, na Mashuka yenye thamani ya Shilingi Milioni 33.1.

Akizungumza Agosti 27,2024 mara baada ya kukabidhiwa Msaada huo katika Kituo cha Afya Kimamba na Shule ya Sekondari Chanzuru Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka amesema Banki ya NMB imekuwa ikishirikiana na Jamii wakati wa changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika wilaya hiyo na kuutaka uongozi na Jamii kwa ujumla kuvitunza vifaa hivyo ili vitumike kwa muda mrefu.

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Ndg. Michael John Gwimile ameishukuru Bank ya NMB kwa msaada huo na kusema kuwa vifaa hivyo vitakwenda kuboresha sekta ya elimu huku akiwataka wanafunzi hususani kidato cha nne kusoma kwa bidii ili kupata ufaulu mzuri katika  Mitihani yao ya mwisho.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Wilfred Sumari amesema Bank ya NMB imekuwa ikijali jamii wakati wa changamoto mbalimbali na kutoa michango mbalimbali pale inapohitajika kufanya hivyo, na kwa upande mwingine ameupongeza Uongozi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Ofisi ya Mkurugenzi  kwa kusimamia vyema utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Naye Meneja wa Bank ya NMB kanda ya Kati Bi. Janeth Shango amesema Bank ya NMB inayo Sera ya kurejesha kwa jamii faida inayopatikana ili kuboresha Huduma muhimu kwa wananchi katika sekta mbalimbali kama vile Elimu, ambapo hutoa madawati kwa shule za msingi, viti na meza kwa shule za Sekondari na vifaa vya kuezekea kwa shule zote, na kwa upande wa Sekta ya Afya  huchangia Vifaa tiba vinavyohitajika katika eneo husika sambamba na kutoa msaada pindi Maafa yanapojitokeza katika maeneo mbalimbali.

Bi. Janeth ameongeza kuwa Bank ya Nmb imeweza kukabidhi  madawati 235 kwa ajili ya shule za Msingi 4 ambazo ni Dakawa Senta 65, Tindiga 60, Malangari 50, Mbigiri 60 pamoja na viti 50 na meza 50 kwa ajili ya shule ya Sekondari  Chanzuru sambamba na vifaa tiba Magodoro 60, Mashuka 60 na Mashine za presha 3 vyenye thamani ya shilingi milioni 33. 1.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa