• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

TANI 485,000 ZA SUKARI KUZALISHWA NCHINI IFIKAPO 2020- WAZIRI MKUU

Posted on: December 7th, 2018

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  amewataka wabia wa sukari ambao ni NSSF pamoja na Jeshi la Magereza kuhakikisha serikali inafikia malengo ya uzalishaji sukari kwa kiwango kinachotarajiwa kwa kuzalisha tani 485,000 ifikapo 2020 ikiwa ni mahitaji ya sukari ya majumbani kwani kwa sasa serikali inatumia fedha nyingi kuagiza sukari nje ya nchi, hivyo njia pekee kufikia malengo hayo ni kuwa na shamba kubwa la miwa, kiwanda na mashine itakayokamua miwa hiyo ili kufanikisha upatikanaji wa sukari.

Majaliwa amesema kuwa kwa sasa kiwango kinachozalisha ni tani 345,000 hivyo ameitaka menejimenti mpya ya NSSF pamoja na bodi mpya ya Mkulazi kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza ambao ni wabia kutoka na mpango thabiti wa kusimamia mashamba ya Mkulazi 1 na 2 yaanze kazi mara moja kwa kuimarisha mifumo yote ya maji ili kuyakusanya yasaidie wakati wa kiangazi, upatikanaji wa mashine za umwagiliaji wakati wa kiangazi.

Aidha amesema ushiriki wa Magereza ni mzuri na amelitaka jeshi hilo kuleta wataalam wa kilimo watakaosimamia kitaalam na kuwa shamba hilo la Serikali liwe shamba la mfano na kuwa na usimamizi wa kutosha ikiwemo upatikanaji wa mashine za uvunaji na usagaji miwa kiwandani na kwamba wanakilosa wawe na mategemeo ya kujifunza kilimo hicho cha miwa ili walime kwa tija.

Aidha amewataka wakazi wa Kilosa na maeneo ya jirani kutumia fursa ya kilimo hicho cha miwa kujifunza na kulima kitaalam kwani vitendea kazi vipo, usimamizi na ushauri utapatikana kupitia wataalam watakaopatikana katika shamba hilo la miwa na kwamba miwa watakayolima itapeleka kiwandani na kuchakatwa jambo litakaloinua uchumi wa mtu mmoja mmoja huku serikali ikipata mapato.

Sambamba na hayo Waziri Mkuu amewaagiza wakurugenzi wote nchini kuhakikisha maafisa kilimo wote nchini hawakai ofisini badala yake wasambae katika kata na vijiji yalipo mashamba ili kuwasaidia wakulima katika namna bora ya kulima kisasa ili waweze kupata tija kupitia kilimo na ametoa wito kwa watumishi wa umma kulima ili kujiongezea kipato kwani ardhi ya kutosha ipo.

Katika ziara yake Waziri Mkuu ameambata na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye ulemavu Mh. Jenista Mhagama pamoja na Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Omary Mgumba.

Akisoma taarifa yake mbele ya Waziri Mkuu Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Mkulazi Hildelitha Msita amesema kuwa baada ya bodi hiyo kuteuliwa aziri mkuu alitoa maagizo kwa bodi hiyo ambapo kwa sehemu kubwa wamyafabyia kazi ikiwemo kumpata  meneja wa mradi, ambapo kwa sasa wanaendelea na usaili wa wafanyakazi upande wa manejimenti, wameshapata wataalam wa kilimo, pia msukumo wao upo katika kupata wakandarasi watakaoweka mitambo ya uhakika, na kwamba ukaguzi wa kampuni umeshafanyika na upembuzi yakinifu wa mradi umefanyika na kwamba licha ya kufanyia kazi maagizo hayo ipo changamoto ya miundombinu ya umeme pamoja na uhakika wa mashine za kiwandani hapo sambamba na uhaba wa mvua kwa mwaka huu.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa