• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Viongozi wa kata wasisitizwa kusimamia vyanzo vya mapato

Posted on: May 13th, 2022

Waheshimiwa madiwani na  Watendaji wa kata wametakiwa kuhakikisha vyanzo vyote vya mapato vilivyopo katika maeneo yao vinakusanywa kwa kadri inavyostahiki ili kuiwezesha Wilaya ya Kilosa kuwa na mapato ya kutosha ili kujiletea maendeleo.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Kilosa Mh. Wilfred Sumari ambapo ametaka kila kiongozi katika eneo lake kusimamia vema vyanzo hivyo ili Wilaya iweze kuendesha shughuli zake pamoja na kujiletea maendeleo.

Akizungumzia zoezi tarajiwa la Sensa ya Watu na Makazi inayotarajiwa kufanyika Agosti 23, 2022 amesema kupitia sensa ndipo takwimu sahihi za kiwilaya hupatikana ambapo ametaka wananchi kuhamasishwa kushiriki zoezi hilo ili kupata takwimu sahihi kwaajili ya kupanga mipango ya maendeleo na upatikanaji wa huduma hizo hupangwa kulingana na idadi ya watu hivyo ni vema ikafanyika hamasa ya kutosha.

Aidha amesisitiza wananchi kuendelea kupata chanjo ya uviko-19 ili kujikinga huku akiwataka viongozi mbalimbali kuendelea kuwahamasisha wananchi ili kufanikisha zoezi la chanjo ya polio kwa watoto chini ya miaka mitano.

Sumari amewaomba viongozi wote kuendelea kushirikiana katika kuijenga Kilosa kwa kusimamia miradi yote inayotekelezwa katika kata mbalimbali huku wakizingatia ushauri wa kisheria na kitaalam pamoja na kusimamia sheria ndogo zilizopitishwa ili zitumike katika vijiji kwa mustakabali wa maendeleo ya wananchi wa Kilosa.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Kisena Mabuba amesisitiza vikao na mikutano itakayofanyika katika kata na vijiji ajenda ya zoezi la sensa ipewe kipaumbele ili kuwajengea wananchi uelewa na hamasa ya kushiriki zoezi hilo huku akibainisha faida za sensa ikiwemo wilaya kupata fedha za maendeleo kwa mujibu wa idadi ya watu, kuinua shughuli za kiuchumi ambapo ametoa rai kwa vijana kuomba nafasi za kazi kwa ajili ya zoezi hilo ambalo mchakato wa maombi mwisho ni Mei 19, 2022.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa