• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WANANCHI WAHIMIZWA KUKATA KADI ZA BIMA YA AFYA - RC MORO

Posted on: October 15th, 2020

Wananchi Wilayani Kilosa na Mkoa wa Morogoro kiujumla wamehimizwa kukata kadi za bima ya afya kwa ajili ya familia zao kwani kadi hizo ni muhimu na zinasaidia kupata matibabu kwa urahisi hata nyakati ambazo mtu anakuwa hana fedha kwa ajili ya matibabu

Rai hiyo imetolewa hivi karibuni na mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare wakati akikabidhi madawati 160 kwa shule za msingi nne,mashuka vipande 3278 na kadi za bima ya afya ICHF na NHIF vyote vikiwa vimefadhiliwa na shirika la World Vision ambalo linafanyua kazi katika Tarafa za Magole na Ulaya kupitia miradi mbalimbali katika sekta ya afya,lishe,maji,elimu na utetezi.

Licha ya kushukuru kwa ajili ya vifaa hivyo Sanare amesema kuwa Serikali inatambua misaada mbalimbali inayotolewa na World Vision lakini pia amelitaka shirika hilo kuendelea kufanya kazi na Halmashauri huku akiliomba kuongeza wigo wa kufanya kazi kwa mapana zaidi katika tarafa nyingine wilayani Kilosa na mkoa wa Morogoro.

Aidha amesema mkoa wa Morogoro umeweka mkakati wa kuwa na shule ya bweni hususani kwa shule za sekondari ili kuwalinda watoto wa kike dhidi ya vishawishi vinavyopelekea kupata mimba wakiwa shuleni na kukatisha ndoto zao ambapo ametaka kuwepo kwa ushirikiano baina ya Serikali na wazazi ili kufanikisha jambo hilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Adam Mgoyi amesema shirika hilo limekuwa mdau namba moja katika kutoa misaada mbalimbali ili kupambana na umasikini ambapo wamekuwa wakitoa elimu katika shughuli mbalimbali zinazojitokeza ikiwemo kutoa elimu ya kilimo cha kisasa na cha kibiashara lakini pia wamekuwa washiriki wazuri katika kukabiliana na majanga mbalimbali kama vile janga la Corona.

Akikabidhi vifaa hivyo kwa Mkuu wa mkoa wa Morogoro kwa niaba ya shirika la World vision Meneja Mradi Elisei Chilala amesema shirika hilo limetoa madawati 160 yenye thamani ya shilingi 13,216,000,kadi za bima ya afya za ICHF kwa watoto 3,000 zenye thamani ya shilingi 15,000,000,kadi za NHIF kwa watoto 10 wenye mahitaji maalumu zenye thamani ya shilingi 504,000 na mashuka vipande 3278 kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi vikiwa na thamani ya shilingi 24,585,000.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa