Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi imeanza zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa awamu ya pili ambapo watendaji wa uboreshaji ngazi ya Halmashauri wametakiwa kuzingatia uadilifu na uaminifu katika zoezi hilo.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi Ndg. Ramadhani Kailima wakati wa mafunzo ya watendaji ngazi ya Halmashauri Wilaya ya Kilosa yaliyofanyika Mei 14, 2025 katika ukumbi wa FDC-Ilonga ambapo amesema uaminifu ni jambo la Msingi huku akiwata kuvitunza vifaa vya BVR wakati wa kutekelezaji wa zoezi hilo.
“Naomba muoneshe na uaminifu Tume inaweza kuendelea nanyi mpaka kwenye kipindi cha uchaguzi “. Alisema Kailima
Kailima amewata watendaji hao kuendelea kuhamasisha na kuelimisha wananchi pamoja na viongozi wa dini katika maeneo mbalimbali umuhimu wa kushiriki zoezi hilo au kutumia fursa hiyo kuhakiki taarifa zao zitakazo wawezesha kushiriki uchaguzi mkuu ifikapo Oktoba, 2025.
Kwa upande wake Afisa Mwandikishaji wa Jimbo la Kilosa na Mikumi Ndg. Betuely Ruhega amesema zoezi hilo linaenda sambamba na uwekaji wazi wa taarifa zilizochukuliwa awamu ya kwanza ambapo tayari ubandikaji wa Daftari katika vituo umefanyika kikamilifu ili wananchi waweze kuhakiki taarifa zao.
Pia Ruhega amewasihi watendaji hao kuzingatia yale yote waliyofundishwa katika mafunzo hayo ili waweze kuwahudumia wananchi kwa weledi unaotakiwa.
Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wameshukuru kwa mafunzo waliyopatiwa na kuahidi kuyatekeleza yale yote waliyofundishwa na pia wamewasihi wananchi kujitokezana kutumia fursa hiyo ya kushiriki katika zoezi la uboreshaji wa Daftari awamu ya pili.
Halmashauri ya Wilaya Kilosa
Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa
Simu: 023 2623093
Simu: 0737847880
Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz
Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa