• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Wazazi hakikisheni watoto wanapata elimu

Posted on: January 30th, 2023

Wito umetolewa kwa wazazi na walezi kuhakikisha watoto wao wanapata elimu kwani kwasasa elimu inatolewa bila malipo, hivyo kila mzazi ahakikishe mtoto anapata fursa ya kupata elimu ambayo itamsaidia katika maisha yake lakini pia kuwalea katika maadili mema kwa kuwarithisha mila na desturi njema ili kuwa taifa lenye sifa njema na maadili mema.

Wito huo umetolewa Januari 30, 2023 na Katibu Mkuu CCM Comrade Daniel G. Chongolo katika ziara yake ya kufatilia utekelezaji wa ilani ya CCM ambapo amewataka wazazi kuhakikisha watoto wao wanapata elimu ambayo inatolewa bila malipo na kwamba mtoto anapopata elimu inamsaidia kupata fursa mbalimbali katika ajira.

Comrade Chongolo amesema kuwa watoto wanapopata elimu ni rahisi kuingia katika sekta mbalimbali ili kujipatia ajira kwani ili kizazi cha sasa kiweze kuwa cha ushindani ni lazima kipate elimu ili kuweza kumudu ushindani wa fursa mbalimbali lakini pia itasaidia kutoa elimu katika familia zao katika masuala mbalimbali ili kujiletea maendeleo yao na familia zao.


Aidha katika ziara yake ametembelea katika shule za sekondari za Maguha na Mikumi  na kuwapatia zawadi ya jezi na mipira miwili toka kwa Mheshimiwa Rais wa awamu ya sita kwa shule zote mbili ambapo pia ametaka kukamilishwa kwa miundombinu ya nishati ya umeme ambayo haijakamilika ili nishati ya umeme iweze kupatikana katika shule ya sekondari ya Maguha ambayo ni mpya, ambapo pia amewapongeza wananchi wa Kilosa kwa juhudi wanazofanya katika kujiletea maendeleo kwa kushiriki shughuli za maendeleo.

Pamoja na hayo ametaka wanakilosa kuunga mkono juhudi mbalimbali zilizofanywa na Serikali kwa kutunza miundombinu mbalimbali iliyopo ndani ya wilaya kwa kuhakikisha inatunzwa ili iweze kutumika kwa muda mrefu huku upande wa mashamba yaliyofutwa na Mheshimiwa Rais amesema Waziri wa kilimo atafika wilayani Kilosa ili kusikiliza wakulima ili yaweze  kutolewa maamuzi sahihi dhidi ya changamoto za wakulima katika matumizi sahihi ya mashamba hayo.

Kwa upande wa mbinge wa jimbo la Kilosa Mh. Prof Palamagamba Kabudi na Mh. Dennis Londo mbunge wa jimbo la Mikumi wameshkuru juhudi mbalimbali zinazofanywa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassani kiwemo kufutwa kwa mashamba 11 na kugawiwa kwa wananchi sambamba na mapinduzi makubwa katika sekta ya elimu, afya,  uboreshwaji wa miundombinu na miradi mbalimbali ya maendeleo na kwamba wanaamini uwepo wa reli ya kisasa utakuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo kwa wananchi wa Kilosa na nchi kiujumla.

Katika ziara yake ya siku moja Comrade Chongolo ametembelea na kukagua miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa shule ya sekondari Maguha, Upanuzi wa kiwanda cha Sukari cha Mkulazi, barabara ya kiwango cha lami Rudewa – Kilosa, Reli ya kisasa ya mwemdo kasi(SGR), shule ya Sekondari Mikumi pamona na kusalimiana na wananchi katika kata za Dumila, Maguha, Mabwerebwere, Ulaya, ,henda na Mikumi.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa