• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MAAFISA ELIMU KATA , WAKUU WA SHULE WAMETAKIWA KUSIMAMIA VEMA MAJUKUMU YAO

Posted on: January 27th, 2024

 

Maafisa Elimu Kata na Wakuu wa Shule Msingi wilayani Kilosa wametakiwa kutekeleza na kusimamia vema majukumu yao na kufanya tathimini ya kina juu ya maendeleo ya kielimu katika shule zao hasa upande wa kitaaluma ili kuleta matokeo chanja kama ilivyokusudiwa.

Hayo yamebainishwa January 26, 2024 katika ukumbi wa Mamboya kata ya Kilosa Mjini na Mkuu wa divisheni ya Elimu Msingi Bi Zakia Fandey katika kikao kazi cha tathimini ya mitihani ya darasa la nne na darasa la saba 2023, ambapo pia ni kikao cha kwanza cha utekelezaji Elimu Msingi.

Ameeleza kuwa endapo Afisa Elimu na wakuu wa shule wakiongeza bidii katika ufatiliaji wa karibu wataweza kubaini changamoto mbalimbali zinazowakabili wanafunzi na walimu na kuzitatua kwa wakati katika shule zao itaondoa adha ya kushuka kitaaluma na kuleta matokeo au ufaulu wa kiwango cha juu.

Sambamba na hayo amezipongeza baadhi ya shule zilizoingia kumi bora kiwilaya katika mitihani ya darasa la saba kwa ufaulu wa asilimia 77.32 ambapo shule hizo ni kama vile Bichop Chitemo, St. peters clavery, Miyonga, Amani, Kantui, King vision, Kikoboga, Mambegwa, Mabwegere na Ruaha B na kuwataka waongeze jitihada zaidi kwa  kushika nafasi za juu kimkoa mpaka ngazi ya kitaifa pia ameshauri kwa baadhi ya shule ambazo hazikuingia kumi bora wajifunze kupitia shule hizo ambazo ni mfano wa kuigwa.

Pia amesisitiza walimu kuendelea na zoezi la uandikishaji kwa elimu ya awali  katika kata zote 40 na kufikia lengo lilokusudiwa, hivyo ameshauri walimu kuendelea kuhamasisha wazazi kuleta wanafunzi shuleni.

Naye Afisa Elimu watu wazima Richard Mpumilwa amewakumbusha Wakuu shule kutunza mazingira ya shule kwa kupanda miti na maua, kuhakikisha mazingira yanakuwa safi na rafiki kwa mwanafunzi kusoma ili kuzuia magonjwa ya mlipuko kama vile kipindupindu.

Pia ameongeza kuwa ili kupunguza adha ya uchache wa madawati, Afisa Elimu kata wajitahidi kufatilia na kuomba vibali kwa uongozi wa kata kupata vibali vya uvunaji wa miti ili kupata mbao za kutengenezea madawati na kupunguza changamoto za uchache wa madawati katika shule hizo.

Kwa upande wake Katibu Msaidisi wa Tume ya Utumishi ya Walimu Daud Mchillu Amewataka waalimu kuwa waadilifu, kuwa na mahusiano mazuri  katika vituo vyao vya kazi pia kufanya kazi kwa ushirikiano bila kutumia nguvu ya Madaraka vibaya. Pia amewaasa walimu kupunguza kuchukua mikopo katika taasisi mbalimbali au kampuni binafsi zinazokopesha na kusababisha madeni kandamizi na kupelekea udhaifu katika utendaji kazi.

Kikao hicho Kwa pamoja kimeazimia Kuendelea kuwajengea uwezo Walimu kupitia Mafunzo Endelevu ya Walimu Kazini ngazi ya shule, kata na Klasta ili kumudu masomo wanayofundisha pia Kuendelea kubaini wanafunzi watoro na kuwasilisha taarifa kwa Watendaji wa Kata kwa ajili ya kuchukua hatua kwa Wazazi wanaoshindwa kusimamia watoto wao kwenda shule. Pia kuwaelimisha wazazi au walezi wanapotaka kuhama kuzingatia taratibu za uhamisho wa Mwanafunzi.

Aidha Jitihada zaidi zimetakiwa zifanyike ili kuboresha ufaulu wa masomo ya Hisabati, Kiingereza, na Sayansi na Teknolojia.

 

 

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa