• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Bashungwa aagiza ujenzi wa shule ya sekondari Berega kufanyiwa tathmini

Posted on: July 24th, 2022

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikiendelea kuwaletea maendeleo wananchi wa Wilaya ya Kilosa kwa kuipatia miradi mbalimbali ikiwemo miradi iliyotembelewa  na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mh.Innocent Bashungwa ambapo alitembelea ujenzi wa shule ya  Sekondari iliyopo kata ya Berega almaarufu shule ya Sekondari Kabudi ambayo imepelekewa shilingi bilioni moja, ujenzi wa daraja la Berega lenye urefu wa mita 140 litakalogharimu kiasi cha shilingi bilioni 7.9 pamoja na ujenzi wa Kituo cha Afya cha Nhembo kilichopo katika kata ya Mabula kilichopelekewa shilingi milioni 700.


                                                            Baadhi ya majengo ya shule ya sekondari(Kabudi sekondari) katika kata ya Berega ambayo ujenzi unaendelea.

Akiwa katika shule ya Sekondari Kabudi Julai 23, 2022, Mh. Bashungwa amemuagiza Mkuu wa MKoa wa Morogoro Martine Shigela kusimamia kamati mbili zilizoundwa kuangalia matumizi ya fedha shilingi bilioni moja zilizoletwa na Serikali katika shule hiyo kwa ajili ya kidato cha tano na cha sita kama matumizi yake yamefuata taratibu na miongozo iliyopo na kuiwasilisha taarifa ya kamati hizo ofisini kwake, huku akimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kuanza maandalizi ya kuwapokea wanafunzi wa kidato cha tano katika shule hiyoambao wataanza masomo yao mwezi Septemba 2022 kwa kuhakikisha vyumba vya madarasa vinakamika na kuwa tayari kwa matumizi.

                                                                                    Baadhi ya majengo ya ujenzi unaoendelea kituo cha Afya Nhembo kata ya Mabula

Kwa upande wa ujenzi wa kituo cha afya Nhembo katika kata ya Mabula Bashungwa amepongeza ujenzi wa kituo hicho ambacho kitaondoa kero ya wananchi kutembea umbali mrefu kwenda kufata huduma za afya ambapo kwa sasa wananchi hutembea umbali mrefu jambo ambalo limekuwa adha kwa wananchi kwa muda mrefu huku akiwapongeza wananchi wa kata hiyo kwa kushiriki kikamirifu katika ujenzi wa kituo hicho. 

Akiwa katika mradi wa ujenzi wa daraja la Berega ambalo limekuwa changamoto kubwa ya ukosefu wa mawasilianokwa  wananchi wa kata ya Belega kwa muda mrefu na kusababisha vifo vya wananchi Bashungwa  amemtaka mkandarasi anayejenga daraja hilo Nyanza Road Works Ltd kukamilisha kazi hiyo ifikapo mwezi Juni 2023 kama mkataba unavyoonesha ambapo pia amemtaka Meneja wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini TARURA Mkoa wa Morogoro kusimamia ukamilishaji wa mradi huo kwa muda uliopangwa.

Sambamba na hayo amemuagiza Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro kufanya afiti matengenezo ya  maeneo yasiyopitika kiurahisi barabara hiyo ambayo inaunganisha Wilaya ya Kilindi Mkoa Tanga ili yaboreshwe ili daraja hilo liweze kuwa na tija kwa Wilaya za Kilosa na Gairo za Mkoa wa Morogoro na Kilindi na Handeni kwa Mkoa wa Tanga.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akifafanua kuhusu hatua zilizochukuliwa juu ya ujenzi wa shule ya sekondari Kabudi amesema zimeundwa timu mbili zitakazohusika na ukaguzi ili kujiridhisha na manunuzi ya vitendea kazi ikiwa yalifuata kanuni na taratibu, huku kamati nyingine ikijikita upande wa utalaam wa uhandisi.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kilosa Mhe. Profesa Palamagamba Kabudi ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha fedha za miradi hiyo jimboni kwake hususan ujenzi wa daraja la Berega ambalo ni muhimu sana kwa mustakabali wa maisha ya wananchi wa kata ya Berega na kata nyinginezo kwani daraja hilo limekuwa kero kwa wananchi kwa muda mrefu.

.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa