• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KILOSA YAPIGA HATUA YA UTOAJI LISHE MASHULENI KWA ASILIMIA 84.8

Posted on: August 20th, 2025

Katika kikao cha utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa robo ya nne (Aprili–Juni 2025) kilichofanyika Agosti 20, 2025  Wilayani Kilosa, Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka ametoa wito kwa viongozi na watendaji wa kata zote kuongeza juhudi katika kuhamasisha wazazi na walezi kuchangia chakula shuleni.

Kikao hicho kimewakutanisha watendaji wa kata, wataalamu wa lishe, na viongozi mbalimbali kujadili maendeleo ya lishe mashuleni.

Taarifa iliyotolewa imeonesha kuwa baadhi ya kata hazijafanya vizuri katika utoaji wa chakula mashuleni kutokana na changamoto ya viongozi kushindwa kuwashawishi wananchi kuona umuhimu wa kuchangia chakula kwa watoto wao. Mkuu wa Wilaya huyo amesema suala la lishe bora shuleni ni la lazima kwa maendeleo ya elimu na afya za watoto na amewataka wakuu wa shule kuhakikisha chakula kinatolewa kwa usalama na kuwa na virutubisho stahiki.

Afisa Lishe Wilaya ya Kilosa, Elisha Kingu, akitoa taarifa ya viashiria vya lishe, amesema kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaopata chakula shuleni kutoka asilimia 64.03 katika robo ya tatu hadi asilimia 84.87 kwa robo ya nne, jambo linaloonesha mafanikio ya juhudi za uhamasishaji. Hata hivyo, ameongeza kuwa bado kunahitajika juhudi zaidi kuhakikisha shule zote zinatoa chakula.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Bi. Beatrice C. Mwinuka ametoa rai kwa watendaji wa kuwajibika katika maeneo yaowananyoyasimamia kwa kuetekeleza vyema suala la lishe mashuleni kwa asilimia mia moja (100).

“Viongozi ongezeni jitihada na uwajibikaji kusimamia vyema suala la lishe mashuleni “ Alisisitiza Bi. Beatrice

Aidha, Mtendaji wa Kata ya Masanze kwa niaba ya watendaji kata amesema wamepokea maelekezo hayo na wako tayari kuyaleta kwenye vikao vya vijiji ili wazazi waelimishwe juu ya umuhimu wa kuchangia chakula. Wazazi wengi, amesema, huona ni mzigo lakini ukweli ni kwamba ni uwekezaji wa moja kwa moja kwa maendeleo ya watoto wao.

Afisa Kilimo Bi Zena Omary amewataka watendaji kushirikiana na maafisa kilimo katika kuanzisha bustani shuleni kwa shule zisizo na uwezo wa kifedha. Amesema njia hiyo itasaidia kupatikana kwa mboga na mazao ya chakula shuleni kwa gharama nafuu, huku ikiwajengea wanafunzi uelewa wa kilimo cha bustani.

Tangazo

  • TANGAZO LA MAFUNZO YA UDEREVA WA MAGARI, PIKIPIKI NA BAJAJI September 30, 2025
  • TANGAZO LA TOZO September 10, 2025
  • TANGAZO LA KUKODISHA MASHAMBA YA HALMASHAURI September 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA November 23, 2023
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WANANCHI WILAYANI KILOSA WAHIMIZWA KUFANYA UCHUNGUZI WA AWALI WA SARATANI YA MATITI

    October 01, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI NGAZI YA SHULE WATAKIWA KUFANYA TATHMINI KWA KILA HATUA YA UJENZI

    September 28, 2025
  • KILOSA YAFANIKIWA KUCHANJA MBWA WENGI KATIKA WIKI YA KICHAA CHA MBWA

    September 28, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA MAGUHA KUNUFAIKA NA MASHINE YA KUCHUJA ASALI

    September 21, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa