• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

CAMFED yashauriwa kuongeza wigo katika mikoa mingine

Posted on: August 31st, 2022

Rai imetolewa kwa Uongozi wa CAMFED kuongeza juhudi katika kuhakikisha wanaendelea kuifikia jamii hususani kwa mikoa ambayo bado haijafikiwa na huduma zinazotolewa na CAMFED ambapo wametakiwa kuhakikisha msichana anapata elimu ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais katika utoaji wa elimu kwa watoto wa kike.

Rai hiyo imetolewa Agosti 30 mwaka huu na Mkurugenzi wa Idara ya Mafunzo toka Wizara ya Kilimo Mashaka Mdangi wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya kilimo na ujasiliamali kwa washiriki waliofadhiliwa na CAMFED toka mikoa ya Morogoro, Pwani, Tanga na Iringa ambapo mafunzo hayo ya siku kumi yanafanyika katika chuo cha Kilimo Mati Ilonga.

Mdangi amewataka washiriki hao kutoa elimu kwa jamii kile watakachojifunza ili kusaidia wengine kutumia taaluma waliyopata kwa lengo la kupata tija jambo litakalosaidia wao na jamii kunufaika lakini pia jamii watayoihudumia kupata kilicho bora.

Akizungumzia shirika la CAMFED Meneja Mradi Nelly Fute amesema lengo la uwepo wa shirika hilo ni kuhakikisha wanamwezesha mtoto wa kike kupata elimu kwa kumfadhili masomo yake ya sekondari dhidi ya changamoto mbalimbali zinazomkabili katika maeneo mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa sare za shule, usafiri, madaftari  lakini pia kuhakikisha wanafunzi wote wanaofadhiliwa na CAMFED wanajifunza stadi za maisha katika shule za sekondari kupitia program ya Dunia Yangu Bora, huku wanufaika CAMFED wakisaidiwa kuanzisha  na kukuza biashara zao ili wasiwe tegemezi na kwamba wanaishukuru Serikali kwa namna ambavyo imekuwa ikishirikiana nao ikiwemo fursa ya kupata mafunzo katika chuo cha kilimo na kwamba wanaamini mafunzo hao yatawasaidia kujikwamua na kufanya shughuli zao kitaalam zaidi.

Naye Mkufunzi Mkuu wa mafunzo hayo toka Mati Ilonga Mariam Maranda amesema kupitia mafunzo hayo watahakikisha kila mshiriki anakuwa na uwezo wa kuongeza thamani ya mazao anayojishughulisha ikiwemo kuongeza ubora wa mazao, kuongeza mavuno, namna ya kufanya biashara kwa tija pamoja na utafutaji wa masoko ambapo katika mafunzo hayo watatoa elimu katika makundi ya mazao ya mizizi na nafaka, mazao ya mboga mboga na mazao ya viungo.

Kwa upande wake Mkuu wa chuo cha Mati Ilonga Felix Mrisho amesema wamejipanga kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais za utatuzi wa tatizo la ajira kwani kupitia mafunzo hayo yatasaidia kwa  asilimia kubwa kupunguza tatizo la ajira nchini huku mdau wa maendeleo Dkt. Matokeo Kenendy amewataka washiriki hao kuitumia fursa hiyo vizuri kwa kujifunza na kufanyia kazi yale watakayojifunza ili kujiletea maendeleo binafsi na Taifa kwa jumla.  

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WAKUMBUSHWA KUZINGATIA MAADILI

    June 05, 2023
  • Vikundi vilivyopata mikopo vyatakiwa kufanya marejesho kwa wakati

    June 02, 2023
  • Vikundi vilivyopata mikopo vyatakiwa kurejesha kwa wakati

    June 02, 2023
  • Shaka aahidi kushirikisha wananchi utatuzi wa changamoto

    May 31, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa