• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

CCM KILOSA YAIPONGEZA SERIKALI UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: February 23rd, 2024

Pongezi za dhati zimetolewa kwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na raisi wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia wilaya ya kilosa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi mbalimbali ya maendeleo.

Pongezi hizo zimetolowa katika Taarifa ya Mkuu wa wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambayo ilisomwa na Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Sekondari Ndg.  Joseph Kapere kwa niaba ya Mkuu wa wilaya katika Mkutano Mkuu wa Wajumbe wa Halmashauri ya Chama cha Mapinduzi ambao pia wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya wilaya na Taasisi walishiriki mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Mamboya Februari 23, 2024.

Akisoma taarifa hiyo, amesema kuwa kwa kipindi cha Julai hadi Disemba 2023Wilaya imekuwa ikitekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya huduma za kijamii na kiuchumi ambapo katika shughuli hizo, jumla ya shilingi 31,816,595,748.90 zilitumika kutekeleza miradi hiyo ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Kilosa.

Aidha katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo imeelezwa kuwa kulitokea changamoto mbalimbali ikiwemo kuchelewa kwa matumizi ya fedha kutokana na changamoto za kimfumo, kupanda kwa gharama za vifaa vya ujenzi ikilinganishwa na kiasi cha fedha kinacholetwa pamoja na mafuriko yaliyoikumba wilaya ya Kilosa zimesababisha miradi kutokamilika kwa wakati.

Akiwasilisha taarifa ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Kaimu Meneja wa TARURA wilaya ya Kilosa Mhandisi Winston Mnyaga Amesema kuwa miradi kumi inaendelea kutekelezwa zikiwemo barabara, madaraja na makaravati huku miradi mingine ikitarajiwa kuanza ikiwemo ongezeko la Kilometa moja katika barabara ya Kidodi Vidunda itakayogharimu shilingi milioni 700,000,000.

Aidha ameipongeza serikali Pamoja na wabunge wa majimbo yote mawili kwa jitihada zao za kupambana kupata fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo.

Imeelezwa kuwa halmashauri ya wilaya ya kilosa imeweka mikakati ili kukabiliana na changamoto hizo ikiwemo kuunda kikosi kazi ili kufanya ufuatiliaji wa miradi mara kwa mara na kuweka msukumo ili miradi yote iweze kukamilika kwa wakati.

Akitoa salamu za chama cha mapinduzi (CCM), Mwenyekiti wa chama hicho Ameri Mbaraka amewataka wakuu wa Idara na Vitengo kuhakikisha wanashirikiana na chama hicho katika kuitekeleza miradi kwani Raisi Samia anatoa fedha nyingi kwaajili ya miradi hiyo ya maendeleo wilayani humo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa