• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

CCM Kilosa yaadhimisha miaka 45 ya CCM kwa kutoa bati 200 ujenzi zahanati kitongoji cha Kikonga

Posted on: January 27th, 2022

Katika kuadhimisha miaka 45 ya Chama Cha Mapinduzi kupitia Mwenyekiti wa CCM Wilaya Mh Ameir Mbarak chama hicho kimetoa mabati 200 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kitongoji cha Kikonga katika kata ya Kisanga ili kuwasaidia wananchi waishio katika kitongoji hicho ambao hutembea umbali mrefu ili kupata huduma za kiafya.

Akizungumzia maadhimisho hayo Katibu wa CCM Wilaya Comrade Shaban Mdoe amesema chama hicho kimeona vema kutoa mabati hayo ikiwa ni kutia chachu ujenzi huo utakaogharimu shilingi milioni 68 ambao tayari umeshaanza ambapo amesema wananchi wanapaswa kutiwa moyo kwa kile ambacho wameanza huku akitaka uongozi wa kijiji kutazama ujenzi huo kwa jicho la tatu kwa kuunga mkono juhudi hizo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Alhaji Majid Mwanga amesema kwa dhima aliyokabidhiwa na Mheshimiwa Rais atashirikiana na kitongoji hicho kwa kuhakikisha unakamilika ili kuwasaidi a wananchi hao wanaokumbana na adha kubwa ya kutembea umbali wa zaidi ya kilometa 13 ili kufata huduma za kiafya huku akiiagiza Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kuhakikisha katika zahanati hiyo panajengwa nyumba ya daktari.

Naye diwani wa kata hiyo Mh Hassan Kambenga amesema ujenzi huo unaendelea huku zikifanyika juhudi mbalimbali za kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa kushirikisha Halmashauri katika bajeti zake ambapo pia amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kuunga mkono shughuli za maendeleo zinazoendelea katika kata hiyo.

Mganga Mkuu Wilaya Dkt. George Kasibante amesema kwa jitihada kubwa zilizoonyeshwa na wananchi hao zahanati hiyo itasajiliwa kwa mujibu wa taratibu na maandilizi yote kufanyika ya upatikanaji wa vifaa na wataalam kwa ajili ya kutoa huduma za afya na kwamba kwa kadri ujenzi huo unavyoendelea Halmashauri itaendelea kuunga mkono ujenzi huo kwa kushirikisha Serikali Kuu.

Bi Tasiana Mauma na Daniel Bihagara kwa niaba ya wananchi wenzao wamesema kutokuwepo kwa huduma za afya katika kitongoji hicho imekuwa ikipelekea wajawazito kujifungulia njiani lakini pia kutumia gharama kubwa kwenda kufata huduma za afya ambapo wamesema kupitia zahanati hiyo wanaamini itawasaidia kwa matibabu na huduma za uzazi huku wakiiomba Serikali kuwasaidia ili kukamilisha ujenzi huo.

Aidha katika kuunga mkono juhudi za ujenzi huo ambao unaendelea wadau mbalimbali wamejitokeza na kuahidi michango mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu mstaafu wa iliyokuwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Dkt. George Mlingwa ambaye ametoa mifuko 50 ya saruji, Kudra Ally mzalishaji wa mazao ya misitu ametoa mifuko 9 ya saruji na kuahidi kuchana mbao zote zitakazohitajika kwa ajili ya fremu za jengo zima huku kijiji cha Kisanga kikichangia shilingi milioni moja na Bw. Omari akiahidi kuchimba kisima cha maji.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa