• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

CHANGAMOTO ZA KIFAMILIA ZATAJWA KUWA SABABU YA KUCHELEWA KWA UANDIKISHAJI WA WA NAFUNZI KATIKA TARAFA YA MIKUMI

Posted on: January 10th, 2024

Usimamizi mbaya wa wazazi na walezi, wanafunzi kuchelewa kurudi kutoka kwenye mapumziko ya sikukuu za mwisho wa mwaka pamoja na mwitikio mdogo wa elimu zimetajwa  kuwa ni changamoto zinazosababisha baadhi ya wanafunzi katika tarafa ya Mikumi kuchelewa kuripoti shuleni.

Hayo yamebainishwa Januari 8, 2024 na baadhi ya wakuu wa shule za sekondari na msingi mbele ya kamati ya ukaguzi ilipotembelea shule hizo ili kujionea hali ya uandikishaji na upokeaji wa wanafunzi wapya, mahudhurio ya walimu, hali ya miundombinu pamoja na usafi wa mazingira.

“Baadhi ya wanafunzi wanaishi na bibi zao na wengine wanaishi na ndugu zao hivyo ni ngumu kwa ndugu kuifanya shule kuwa kipaumbele, kuna wakati wanafunzi wanakuja wenyewe bila mtu yeyote wa kuwaleta, ukimuuliza anakwambia kuwa yeye anaishi na bibi yake na amekataa kumleta shuleni” amesema Mkuu wa Shule ya Sekondari  Mikumi.

Akiongoza kamati hiyo maalumu ya ukaguzi, Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira Antony Mbisse amesema kuwa kuna haja ya kamati ya shule kwa kushirikiana na viongozi wa dini pamoja na wa serikali za mitaa kuwatangazia wananchi wenye watoto wanaotakiwa kwenda shule wawapeleke shule ili wapate haki yao ya msingi kwani mpaka sasa hali ya uandikishaji hairidhishi.

Katika hatua nyingine amewataka walimu wakuu pamoja na wakuu wa shule za sekondari kuwapokea watoto hata wale ambao hawajakamilisha mahitaji kama vile sare za shule pamoja na vifaa vya kufanyia usafi kwa wale wanaoanza kidato cha kwanza.

Ameongeza kuwa kuna haja ya walimu wanaohusika na masuala ya ushauri nasaha kujiwekea utaratibu wa kukaa na wanafunzi wanaojiunga na shule hizo ili kubainisha changamoto za kifamilia na kijamii zinazosababisha mkwamo wa elimu kwa wanafunzi hao na kuzipatia ufumbuzi

Kamati hiyo imetembelea shule ya msingi, Mikumi, Ruaha A, Ruaha B pamoja na sekondari za Mikumi na Kidodi ambapo kwa shule ya Sekondari Mikumi wameripoti wanafunzi 71 kati 556 waliopangiwa kujiunga na shule hiyo ikiwa ni asilimia 13 pekee, kwa upande wa shule ya Sekondari ya Kidodi wameripoti wanafunzi 96 kati ya 547 waliopangiwa shule hiyo.

Kwa shule ya Msingi Ruaha A walikadiria (maoteo) kupokea wanafunzi mia moja kwa darasa la awali  ambapo wameandikishwa wanafunzi 32 pekee na kwa darasa la kwanza wameandikishwa wanafunzi 49 kati wanafunzi mia moja waliokadiriwa kuandikishwa, Shule ya Msingi Ruaha B wameandikishwa wanafunzi 190 kati wanafunzi 200 waliokadiriwa kuandikishwa kwa darasa la awali na darasa la kwanza.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa