• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

CHINA ESTATE REKEBISHENI MAZINGIRA YA KIAFYA - WAZIRI MHAGAMA

Posted on: August 1st, 2019

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia  Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye ulemavu Mh. Jenista Mhagama Julai 31 mwaka huu ameigiza kampuni ya China Estate kuhakikisha inaweka mazingira bora ya kiafya katika nyumba za zamani za wafanyakazi wa kiwanda hicho hususani suala la vyoo ambavyo kwa sasa vimejaa na kusababisha wafanyakazi hao kuwa hatarini kiafya.

Jenista ametoa agizo hilo alipotembelea kiwandani hapo ambapo amesema kuwa uongozi wa kampuni hiyo unapaswa kuhakikisha kabla ya tarehe 20/08/2019 vyoo hivyo viwe safi na salama kwa matumizi ya wafanyakazi wanaoishi katika nyumba hizo lakini pia ameagiza uwepo wa vitendea kazi na vifaa kinga kwa wafanyakazi ikiwemo vizuia vumbi, gloves, mabuti na visanduku vya huduma ya kwanza ambapo tarehe 20/08/2019 ukaguzi utafanyika kuhakiki utekelezaji wa maagizo hayo.

Pamoja na maagizo hayo Mhagama ameupongeza uongozi wa kampuni hiyo kwa kujenga nyumba nyingine mpya kwa ajili ya wafanyakazi sambamba na kuwaruhusu wafanyakazi wa kiwanda hicho kufanya shughuli zao za kilimo katika maeneo ya kiwanda ili kujiongezea kipato pamoja na kuwaruhusu uwepo wa wakulima wa nje wa zao la mkonge.

Aidha ametoa rai  kwa uongozi kuanzisha viwanda vingine kwa ajili ya bidhaa mbalimbali ili kwenda sambamba na juhudi za Mheshimiwa Rais Jonh Joseph Magufuli ya kuwa na Tanzania ya viwanda kwani eneo la kiwanda hicho ni kubwa hivyo linakidhi ongezeko la viwanda vingine.

Pamoja na hayo amewahamasisha wafanyakazi wa kiwanda hicho kuwa na mshamba yao ya ziada ili kujiongezea kipato badala ya kutegemea mshahara toka kwa mwajiri wakati fursa ya kutumia maeneo katika kiwanda hicho ipo lakini pia muda wa kufanya shughuli zao upo huku akiwasisitiza kujiunga katika vyama vya ushirika.

Licha ya hayo ametoa wito kwa wawekezaji wote nchini kuhakikisha wanafuata sheria kama inavyostahiki  huku akisisitiza wafanyakazi wote nchini kutambua haki zao lakini pia kutimiza wajibu wao kwa kadri inavyostahiki.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WAKUMBUSHWA KUZINGATIA MAADILI

    June 05, 2023
  • Vikundi vilivyopata mikopo vyatakiwa kufanya marejesho kwa wakati

    June 02, 2023
  • Vikundi vilivyopata mikopo vyatakiwa kurejesha kwa wakati

    June 02, 2023
  • Shaka aahidi kushirikisha wananchi utatuzi wa changamoto

    May 31, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa