• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

CWT KILOSA YAWEKA HISTORIA UNUNUZI WA BASI KWA MKOA WA MOROGORO

Posted on: March 16th, 2024

Chama Cha Walimu wilayani Kilosa kimepongezwa kwa juhudi mbalimbali ambazo imekuwa ikifanya katika kujiletea maendeleo ikiwemo tukio la kihistoria la ununuzi wa chombo cha usafiri wa basi dogo ikiwa ni wilaya ya kwanza kwa mkoa wa Morogoro.

Pongezi hizo zimetolewa Machi 15, 2024 wakati wa uzinduzi wa basi pamoja na sera ya matumizi ya basi hilo uliofanywa na Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Ndg. Alto Mbikiye  kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, ambapo amepongeza chama hicho kwa hatua hiyo ambayo ni mfano wa kuigwa na wilaya nyingine zenye nia ya kujiletea maendeleo.

Akionyesha kufurahishwa kwake na tukio hilo Mbikiye amesema kuwa uwepo wa basi hilo utakuwa chachu ya maendeleo kwa chama hicho, huku akitaka sera ya matumizi ya usafiri huo kusimamiwa vizuri kwa kuepuka upendeleo hususani katika matumizi na kwamba sera ikiheshimiwa na kila mmoja itaepusha migogoro na badala yake itawajenga pamoja kwa umoja, ushirikiano, upendo, mshikamano na amani ndani ya chama.

Akizungumzia suala la malimbikizo ya madai mbalimbali ya walimu Mbikiye amesema Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni sikivu na kadri fedha inapopatikana inaendelea kupunguza madeni mbalimbali yakiwemo madeni ya fedha za wastaafu na likizo hivyo walimu wote na watumishi wenye madai waendelee kuwa na subra madai yote yaliyohakikiwa yatafanyiwa kazi.

Richard Shagungu ambaye ni Mwenyekiti wa Chama Cha Walimu Kilosa amewapongeza wanachama wenzake kwa kufikia makubaliano ya ununuzi wa basi hilo ambayo yamefuata taratibu zote za vikao vya ridhaa na manunuzi huku akisema kuwa anaamini kupitia chombo hicho kitazidi kuwaweka pamoja kama chama na kwamba wanatarajia kuunda kamati maalumu itakayosimamia vema matumizi ya usafiri huo.

Aidha licha ya kuipongeza Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa ombi kwa Serikali kulitazama kwa upya suala la kikokotoo ambalo limekuwa changamoto kubwa kwa wastaafu hivyo ni vema ukawekwa utaratibu wa kuhakikisha watumishi wa umma pindi wanapostaafu wapatiwe mafao yao yote ya kustaafu ili kuwaweka katika mazingira mazuri kimaisha, huku akipongeza uongozi wa Halmashauri kwa kufanyia kazi kilio chao cha muda mrefu kwa kutenga fedha za matibabu.

Naye Katibu wa CWT Kilosa Andrew Ngazu amewashukuru wanachama wote wa CWT kwa ushirikiano walioutoa katika kusimamia azimio la ununuzi wa chombo hicho ambalo walijiwekea na kulitimiza ndani ya mwaka mmoja jambo ambalo kwao limekuwa ni fahari kubwa ambapo amebainisha kuwa wanachama waliliridhia kutotumia 15% ya mapato yao ya uendeshaji wa shughuli zao kwa lengo la kufanikisha azimio hilo ambapo matumizi ya basi hilo yatazingatia sera inavyosema na kwamba sera hiyo itaendelea kuboreshwa kwa maslahi ya chama hicho ili kujijenga zaidi.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa