• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

DAS KILOSA AKABIDHI MIPIRA 240 KWA SHULE ZA MSINGI

Posted on: April 2nd, 2024


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)  kupitia Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Morogoro wamekabidhi mipira 240 katika shule za msingi  sita (6) kwa lengo la kuinua na kukuza vipaji kwa wanafunzi mashuleni kuanzia ngazi ya  chini ili kuboresha  Tasnia ya mchezo wa mpira wa miguu kwa ngazi ya kimataifa.

Hayo yameelezwa leo na Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilosa Bi. Salome Mkinga   wakati wa hafla ya kukabidhi mipira hiyo kwa walimu iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Kilosa.

Bi. Salome amesema kuwa  Serikali imeona vema kukuza vipaji vya michezo kuanzia mashuleni ambapo muwajibikaji wa kukuza vipaji hivyo na kuviendeleza  atakuwa  mwalimu wa michezo ambapo hatua hii italeta tija katika kukuza vipaji vya watoto wakiwa bado wadogo.

Bi. Salome ametoa Rai kwa walimu na viongozi wa michezo katika ngazi ya wilaya kushirikiana kwa pamoja katika kufanikisha juhudi za serikali na kusema kuwa suala la michezo ni ajira pia ni sehemu ya kujipatia kipato, hivyo ni jukumu lao kuhakikisha wanasimamia vyema  kukuza vipaji vya wanafunzi ili kuleta matokeo chanya kama ilivyokusudiwa.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Morogoro (MRFA)  Bw. Pascal Kihanga amesema kuwa serikali kupitia Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wameweza kutoa mipira hiyo mashuleni lengo ni kukuza vipaji vya watoto kuanzia ngazi ya chini  wakiwa na umri mdogo kuanzia miaka saba badala ya kuwafundisha vijana wenye umri mkubwa ambapo baada ya kufundishwa na kujua kucheza mpira tayari  umri wao wa kucheza unakuwa umeisha.

Kihanga amewata walimu kuwa wasimamizi wazuri na kuleta matokeo chanya na  watoto watakaofanya vizuri baada ya ufuatiliaji watachukuliwa na kupelekwa kwenye vituo maalum vya mafunzo ambavyo vipo Tanga na Kigamboni.

Sambamba na hayo ameongeza kuwa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Morogoro (MRFA) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kitatoa mafunzo kwa walimu ili kuwajengea uwezo wa kufundisha mpira wa miguu watoto wadogo .

Kwa upande wake Afisa Utamaduni Bi. Paula Katololo amesema michezo hiyo itachezwa kwa kushirikisha jinsia zote mbili wa kike na kiume ambapo mipira hiyo 40 iliyotolewa kwa shule moja itatumika kwa usawa mipira 20 kwa wanafunzi wa kike na 20 kwa wanafunzi wa kiume.

Katika hatua hiyo ya awali shule zilizoanza kupewa mipira hiyo ni pamoja na shule ya msingi Mazinyungu, Ruhembe, Mbamba, Ifunde, Matongole na Ng'ole.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa