• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

DC- AAGIZA VISIMA VIFUPI VIFUKIWE

Posted on: August 14th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam I. Mgoyi ametoa agizo kwa wananchi wote wa Tarafa ya Kilosa Mjini kuhakikisha visima vifupi vyote vilivyopo katika makazi ya yao vinafukiwa ndani ya siku kumi na nne  kuanzia tarehe 14/08/2018 baada ya kubainika visima hivyo kuwa na kutu ambayo ina madhara kwa wananchi hao ikiwemo kupatwa na kansa ambapo amesema serikali ya awamu ya tano haiko tayari kuona wananchi wakiangamia huku viongozi wakiangalia.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya kwenye mkutano wa hadhara katika Tarafa ya Kilosa Mjini na kusema wamiliki wote wa visima hivyo wanapaswa kuvifukia ndani ya siku kumi na nne na kwamba atakayekaidi agizo hilo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake kwani mamlaka ya maji ipo tayari kuwasaidia wananchi namna ya kupata maji na watawaunganishia bure baada ya kukamilisha maelekezo.

’’Lakini pia niseme na nyinyi wazazi ambao watoto wenu wa kike wakibebeshwa mimba mna mtindo wa kuwaficha wanaohusika na mimba hizo kitendo ambacho sio kizuri kwani elimu ni haki ya msingi ya kila mtoto hasa katika awamu hii ya tano ambapo elimu inatolewa bure, hivyo mzazi atakayebainika kushirikiana na mtuhumiwa wa mimba hatua stahiki zitachukuliwa dhidi yake kwani tendo la kumficha mhusika ni dhahiri linaonyesha kushiriki kupoteza ndoto za mtoto wa kike kupitia elimu ambayo angepaswa kuipata’’. Mgoyi ameongeza.

Sambamba na hayo amewatahadharisha wazazi na wananchi wanaolalamikia suala la upendeleo wa ajira katika kampuni ya Yapi Merkez ambapo amesema hakutakuwa na upendeleo wa aina yoyote kwani watakaofaidika na ajira toka kampuni hiyo ni wale wenye sifa na vigezo stahiki ambao watakuwa wamefanya vema katika usaili wa nafasi mbalimbali zilizotangazwa.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Program ya Dunia Yangu Bora Yawa Chachu Njema Mashuleni

    August 11, 2022
  • Maonesho ya Nane Nane kuwa Endelevu

    August 08, 2022
  • Fanyeni Maonesho ya Nane Nane kuwa na tija - Mh. Pinda

    August 04, 2022
  • RUWASA, MORUWASA shirikianeni na taasisis nyingine kuibua vyanzo vya maji

    August 02, 2022
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu:

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa