• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

DC KILOSA- MARUFUKU SHUGHULI ZA KIBINADAMU MTO MKUNDI

Posted on: November 26th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ametoa wito kwa wananchi wa kata ya Mbigiri kusitisha shughuli zozote za kibinadamu kutokana na mabadiliko yaliyojitokeza kutokana na shughuli hizo ikiwemo kilimo na shughuli nyinginezo, hivyo kusababisha mto Mkundi kubadili njia yake na kuleta madhara ya mafuriko yaliyopelekea baadhi ya maeneo katika kata hiyo kuharibiwa na maji na kusababisha madhara ikiwemo kuanguka kwa baadhi ya nyumba na wakazi wake kukosa malazi.

Mgoyi amesema hayo Novemba 25  mwaka huu wakati alipowatembelea wananchi wa Mbigiri kwa ajili ya kuwapa pole ambapo amesema kuwa kutokana na mabadiliko ya shughuli za kibinadamu mto Mkundi umeharibika  ambapo hali hiyo imetokana na kutozingatiwa kwa sheria ambayo inasema mita sitini kusiwe na shughuli za kibinadamu lakini kutokana na kutofuatwa kwa sheria hiyo kumesababisha madhara hayo, hivyo shughuli za kibinadamu zisifanyike tena ili kuepuka madhara makubwa yanayoweza kujitokeza.

Pamoja na hayo amesema Mto Mkundi umejaa mchanga na kwamba mto huo unatembe juu ya mchanga na kwamba awali mto huo haukuwa na makazi ya watu wengi lakini kutokana na shughuli za kibinadamu kumekuwa na ongezeko la watu ambao wamekuwa wakiendelea na shughuli za kibinadamu hasa katika kingo za mto jambo lililopelekea madhara yaliyojitokeza na kwamba endapo shughuli za kibinadamu zikiendelea zitaleta madhara makubwa kwani mto huo hauna njia maalum, hivyo kila mwananchi anao wajibu wa kulinda mto huo na kupanda matete ili kuepusha madhara.

Aidha ametoa wito kwa viongozi wote wa serikali za vijiji na watendaji wa kuajiriwa kusimamia sheria ili kuepusha madhara ambayo yanaweza kujitokeza kwa wananchi na kwamba kiongozi yoyote atakayeshindwa kusimamia sheria hatua kali zitachukuliwa dhidi yake, pia amesema ni wajibu wa viongozi na wananchi hao kuwa walinzi wa maeneo hayo kwa kuhakikisha maeneo hayo yanasimamiwa kwa kufuata sheria kwa kutofanya shughuli za kibinadamu kwenye kingo za mto.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale amesema kutokana na madhara hayo watendaji wa vijiji na kata katika maeneo yaliyoathirika wanaendelea na tathmini ili kubaini madhara yaliyojitokeza lengo ikiwa ni kupata kiwango cha madhara yaliyojitokeza kwa ajili ya kuchukua hatua zaidi lakini pia ametoa rai kwa wananchi wa Mbigiri kuchukua tahadhari ya kutosha  kwani mto Mkundi hauna njia moja hivyo ni vyema maeneo hayo yakatumika zaidi kwa ajili ya shuguli za kilimo na kuepuka kuishi katika maeneo hayo kwa kupata makazi mbadala.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa