• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

SERIKALI YASHIRIKIANA NA CAMFED KUFIKISHA HUDUMA YA MAJI SHULE ZA MSINGI KILOSA

Posted on: September 3rd, 2025

Wananchi  Wilayani  Kilosa  wametakiwa kuilinda na kuitunza miundombinu mipya ya maji ili iweze kudumu kwa muda mrefu itakayowanufaisha wanafunzi na jamii kwa ujumla.

Kauli hiyo imetolewa Septemba 3, 2025 na Mkurugenzi kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI Bi. Beatrice Kimoleta, wakati wa uzinduzi wa kisima cha maji safi katika Shule ya Msingi Kitungu, Kata ya Mtumbatu, ambapo amesema mradi huo umefadhiliwa na Shirika la CAMFED linalojihusisha na kampeni ya elimu kwa mtoto wa kike.

Bi. Beatrice ambaye alikaimu nafasi ya Naibu Katibu Mkuu Elimu kutoka TAMISEMI, Mhe. Atupele Ambwene, ameeleza kuwa ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha  miundombinu  inakuwa na usimamizi hivyo amewataka  wazazi na walezi kuunda  kamati zitakazo simamia visima hivyo na kuhakikisha kushughulikia usafi, uendeshaji, matengenezo na matumizi sahihi ya vyanzo hivyo vya maji.

Pia ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kushirikiana na Taasisi binafsi katika kuleta maendeleo kwa wananchi, hususani kupitia Sekta ya Elimu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Bi. Beatrice C. Mwinuka amesema Wilaya ya kilosa imekuwa na changamoto ya upatikanaji wa maji na kupelekea kukwamisha shughuli za ujenzi hivyo amewataka wasimamizi wa mradi kuweka utaratibu mzuri utakaowezesha vijiji vya jirani kupata maji kupitia mradi huo.

Aidha, ameongeza kuwa  mradi huo ni sehemu ya mpango mpana uliohusisha ujenzi wa visima 10 katika shule za Msingi 10 zilizopo katika kata ya Mtumbatu, Mvumi, Mang’ula, Magomeni, Masanze, Mkwatani, Mabwerebwere, Chanzuru, Mamboya na Mbumi.

Naye Mkurugenzi wa CAMFED Tanzania Bi. Nasikiwa Duke amesema  kupitia kisima hicho kitasaidia shughuli mbalimbali ikiwemo upandaji miti, upatikanaji wa chakula shuleni lakini pia itaondoa adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kutafuta maji.

Ameongeza kuwa kisima hicho ni cha kisasa kinachotumia mionzi ya jua kuvuta maji chini na kupandisha juu ya vyombo vya kuhifadhia maji ambapo mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 305 hadi kukamilika katika shule zote.

Tangazo

  • TANGAZO LA MAFUNZO YA UDEREVA WA MAGARI, PIKIPIKI NA BAJAJI September 30, 2025
  • TANGAZO LA TOZO September 10, 2025
  • TANGAZO LA KUKODISHA MASHAMBA YA HALMASHAURI September 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA November 23, 2023
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WANANCHI WILAYANI KILOSA WAHIMIZWA KUFANYA UCHUNGUZI WA AWALI WA SARATANI YA MATITI

    October 01, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI NGAZI YA SHULE WATAKIWA KUFANYA TATHMINI KWA KILA HATUA YA UJENZI

    September 28, 2025
  • KILOSA YAFANIKIWA KUCHANJA MBWA WENGI KATIKA WIKI YA KICHAA CHA MBWA

    September 28, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA MAGUHA KUNUFAIKA NA MASHINE YA KUCHUJA ASALI

    September 21, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa