• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAZAZ/WALEZI WAHIMIZWA KUCHANGIA CHAKULA SHULENI ILI KUONGEZA UFAULU NA KUPUNGUZA UTORO

Posted on: September 3rd, 2025

Katika kuhakikisha wanafunzi wanapata haki yao ya msingi ya kujifunza katika mazingira bora, Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imeendelea kuhimiza ushiriki wa jamii, hususani wazazi, katika kuchangia chakula shuleni ili kuhakikisha wanafunzi wanapata mlo wa mchana unaowasaidia kiafya na kielimu.

Wito huo umetolewa Septemba 3, 2025 katika  kikao cha kawaida cha utekelezaji wa afua za lishe kwa kipindi cha robo ya nne kwa mwaka  wa  fedha 2024/2025 kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa.

Mwenyekiti wa kikao hicho, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Bi. Grace L. Nyabange, amezitaka Divisheni na Vitengo zinazohusika na masuala ya lishe ikiwemo Divisheni ya Kilimo, Biashara, Fedha, Elimu Msingi na Sekondari kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuhakikisha wanayafikia malengo waliojiwekea kuwa kila wanafunzi shuleni anapata chakula bora.

Aidha ametoa msisitizo kwa wazazi kutambua kuwa uchangiaji wa chakula au fedha ni sehemu ya uwekezaji kwa maendeleo ya watoto wao na taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari Daniel Kisoso ameeleza kuwa utoaji wa chakula shuleni umeleta matokeo chanya katika shule nyingi, ikiwa ni pamoja na kupunguza utoro wa wanafunzi na kuongeza ufaulu huku akitoa mfano wa shule zinazotekeleza mpango huo ambazo zimeonyesha mabadiliko makubwa kitaaluma.

Naye Afisa Lishe wa Wilaya, Elisha Kingu, amesema kikao hicho kimekuwa sehemu muhimu ya tathmini na kujifunza kuhusu hali ya lishe wilayani humo. Amesema kuwa kwa robo ya mwisho, kata zote zimefanya vizuri, lakini akasisitiza haja ya idara zote kuendelea kushirikiana ili mafanikio hayo yawe endelevu na kwamba watoto wanapaswa kupatiwa lishe kamili yenye virutubisho muhimu badala ya chakula cha aina moja.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI KILOSA DC June 06, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • SERIKALI YASHIRIKIANA NA CAMFED KUFIKISHA HUDUMA YA MAJI SHULE ZA MSINGI KILOSA

    September 03, 2025
  • WAZAZ/WALEZI WAHIMIZWA KUCHANGIA CHAKULA SHULENI ILI KUONGEZA UFAULU NA KUPUNGUZA UTORO

    September 03, 2025
  • KILOSA YATOA MILIONI 541.3 MIKOPO YA 10 % KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

    August 27, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KWA KASI KATIKA JIMBO LA KILOSA NA MIKUMI

    August 21, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa