• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

DC SHAKA AMEVITAKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUSIMAMIA HAKI ILI KUEPUSHA UVUNJIVU WA AMANI

Posted on: March 16th, 2024


Mkuu wa wilaya ya kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kusimamia taratibu na sheria zilizopo kuhakikisha haki inatendeka ili kuimarisha ulinzi na usalama kwa wananchi na mali zao.

Rai hiyo ameitoa  katika mkutano wa hadhara uliofanyika 16 Machi, 2024 katika Kitongoji Cha Mbegesela Kijiji cha Ihombwe kata ya Mikumi ambapo  Mhe. Shaka amesikiliza kero mbalimbali kama vile mgogoro wa ardhi kati ya Bw. Ndemeka na baadhi ya wananchi katika kitongoji cha Mbegesela.

Akitolea ufafanuzi wa mgogoro huo unaohusisha mwingiliano wa mipaka ambapo Bw. Ndemeka anatuhumiwa kuingia kwenye mipaka ya wananchi wenzake na kujimilikisha ardhi kinyume na sheria , Mhe. Shaka amesema  kuwa ni vema kuheshimu sheria, taratibu na maamuzi yaliyokwisha fanywa na viongozi waliopita na si kwenda kinyume kwa kuibua upya migogoro ya miaka ya nyuma ambayo tayari ilishasikilizwa na kutatuliwa na viongozi waliopita badala yake kujikita zaidi katika uzalishaji  na kushirikiana katika shughuli za  maendeleo.

Ameongeza  kuwa ili migogoro  ya ardhi iweze kuisha, kila mwananchi anawajibika kumiliki ardhi aliyonayo kisheria  ili kuepuka migogoro inayopelekea vitendo vya uvunjifu wa amani katika maeneo yao.

Pia Mhe. Shaka amewataka wananchi kutoa ushirikiano wao kwa jeshi la polisi kwa yeyote anayekwenda kinyume na sheria na kusababisha vitendo vya uvunjivu wa amani  sheria kali zichukuliwe ikawe fundisho kwa wengine.

Sambamba na hayo Mhe. shaka ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia kata ya Mikumi fedha kiasi cha shilingi bilioni 1.28 kwa ajili ya Ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwemo Daraja na shule ya Sekondari.

Pia amempongeza mbunge wa Jimbo la Mikumi Mhe. Dennis Londo  kwa juhudi zake za kuleta mnara wa Mfilisi ambao ukikamilika utatua changamoto ya mawasiliano katika kata hiyo.

 

Tangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA WAHE. MADIWANI May 22, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WAUGUZI WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAHALI PA KAZI

    May 30, 2025
  • WAHE. MADIWANI WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 30, 2025
  • KILOSA YAJIPANGA KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

    May 28, 2025
  • VITENGO VYA HABARI SERIKALINI VIIMARISHWE KWA KUFANYA MAWASILIANO YA KIMKAKATI

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa