• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

DC Shaka asisitiza wanafunzi kuripoti shuleni kwa wakati

Posted on: January 10th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Comrade Shaka H. Shaka amewataka walimu wakuu wote wa shule za sekondari kushirikiana na viongozi wa kata zote ikiwemo madiwani, watendaji wa kata na vijiji, wenyeviti pamoja na wazazi kuhakikisha wanafunzi wote wanaostahili kuanza kidato cha kwanza wanaripoti shuleni na kuanza masomo haraka iwezekanavyo.

Agizo hilo limetolewa Januari 09/01/2024 wakati akifanya ziara ya ufatiliaji mapokezi ya kaguzi wa mahudhurio ya wanafunzi walioripoti shule na kuanza masomo hususani kwa kidato cha kwanza, elimu ya awali na darasa la kwanza ambapo ametaka viongozi wa kata na vijiji vyote kushirikiana kwa pamoja kuhakikisha wanafunzi wote wanaripoti na kuanza masomo ili watoto wote waweze kupata elimu inavyostahiki.

Shaka katika ziara yake ametembelea shule ya msingi na sekondari  Parakuyo na shule ya sekondari Mkulo ambapo ametoa onyo kwa mzazi au mlezi yoyote atakayebainika kumtorosha mtoto hususani wa kike kwa lengo la kumuozesha kwani hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake,huku akisisitiza wazazi au walezi kuacha mara moja tabia ya kufanya uhamisho feki ambapo kila uhamisho utafuatiliwa na ikibainika kuwa ni feki hatua stahiki zitachukuliwa kwa yoyote atakayehusika kwani tayari kuna baadhi ya wazazi wameanza kupokea mahari jambo ambalo limeshaanza kufanyiwa kazi na kuwa Serikali haitosita kuchukua hatua kwa mzazi atakayebainika kutaka kuhujumu upatikanaji elimu wa watoto.

                                                                                                                                                                                                          Ujenzi wa hostel kwa ajili ya wanafunzi


Aidha ameuagiza uongozi wa kata ya Parakuyo kushirikiana na Idara ya ardhi kuhakikisha ifikapo tarehe 15/01/2024 eneo la mipaka ya shule ya sekondari Parakuyo inapimwa na kuainishwa vizuri ili kuepusha migogoro ya watu kuvamia maeneo ya Serikali huku akimshkuru Mheshimiwa rais Dkt. Samia suluhu Hassan kwa zaidi ya shilingi bilioni 3.5 zilizoelekezwa katika sekta ya elimu ambapo pia amewashukuru wabunge wa majimbo yote mawili Kilosa na Mikumi kwa ushirikiano na juhudi ambazo wamekuwa wakizifanya ili kuiletea Kilosa maendeleo.

Naye Katibu Mwenezi Jafari Kunambi kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Kilosa amewataka viongozi wote wa CCM ndani ya kata zao kuendelea kuhamasisha jamii wanazoishi nazo kuona umuhimu wa elimu ili watoto wote waweze kupata elimu huku akitaka viongozi ngazi ya kata kuwa wepesi kutatua migogoro kwa wakati katika maeneo yao kwani kuna migogoro ambayo ipo ndani ya uwezo wao wanayopaswa kuitatua badala ya kusubiri viongozi wa ngazi za juu.

Kwa upande wake diwani wa kata ya Parakuyo Mh Ibrahim Kalaita ameiomba Serikali kupitia mradi wa BOOST kuongeza shule nyingine ya msingi katika kijiji cha Mkata Station ili kuwapunguzia adha ya wanafunzi ya kutembea umbali mrefu, kwani kwasasa wanafunzi wa kijiji cha Mkata wanatumia shule ya msingi Parakayo ambayo kwasasa imekuwa na wanafunzi wengi.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa