• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

DC SHAKA AWATAKA WAFANYABIASHARA WA SUKARI WILAYANI KILOSA KUFUATA BEI ELEKEZI ILIYOPANGWA NA SERIKALI

Posted on: February 22nd, 2024

Mkuu wa wilaya ya kilosa Mhe. Shaka Hamdu  Shaka amewataka walanguzi na wafanyabiashara ya sukari  kufuata bei elekezi iliyopangwa na serikali ili kuweka usawa kwa wananchi wote kupata bidhaa hiyo muhimu.

Mhe. Shaka ameyasema hayo Februari  22, 2024 katika kikao cha Baraza la Ushauri Wilaya (DCC) kilichofanyika katika ukumbi wa FDC Ilonga ambapo amesema hatua kali za kisheria zitafuatwa endapo wafanyabiashara hao watakiuka tamko la serikali.

Mhe.Shaka amewataka wananchi kutoa ushirikiano wao kwa jeshi la polisi pamoja na kamati ya ulinzi na usalama kwa kutoa taarifa kwa wakati endapo watabaini kuna wafanyabiashara wanaokiuka kufuata bei hiyo elekezi ili hatua za kisheria zichukuliwe.

Ameongeza kuwa kamati ya ulinzi na usalama inaendelea kufatilia suala hilo kwa ukaribu mkubwa ambapo wamefanya ziara ya kutembelea maduka katika maeneo mbalimbali kuona mabadiliko ya bei ya bidhaa hiyo pamoja na kufanya ziara ya kutembelea kiwanda cha sukari cha Mkulazi ambacho kinaendelea na uzalishaji wa sukari pamoja na changamoto zilizopo katika mashamba ya miwa kujaa maji kutokana na mvua zilizonyesha na kusababisha mazingira kutokuwa rafiki katika mashamba hayo.

Sambamba na hayo ameeleza kuwa kamati ya ulinzi na usalama imefikia maamuzi ya pamoja na kiwanda cha sukari cha Mkulanzi kwa kuwatumia mawakala wa usambazaji wa sukari katika  ukanda wa kilosa na kipaumbele cha kwanza  ni wananchi wa kilosa kusambaziwa sukari hasa katika maeneo ya dumila, kilosa kati, ulaya  na  maeneo jirani.

Aidha Mhe. Shaka ameongeza kuwa kamati ya ulinzi na usalama kwa kushirikiana na wananchi wanaendelea kusaidiana kupunguza migogoro ya wakulima na wafugaji ambapo kwa mwaka 2023 hakuna vifo vilivyosababishwa na migogoro ya wakulima na wafugaji ukilinganisha na miaka nyuma. Sambamba  na kutatua migogoro ya ardhi kwa kuandaa program maalum ya kuelimisha wananchi juu ya kumiliki ardhi kisheria.

Kwa upande mwingine amewasisitiza Watumishi wa Halmashauri kila mmoja kwa nafasi yake kuwajibika ili kuweza kuwasaidia viongozi kutekeleza mipango inayopangwa katika kuwaletea Wanachi maendeleo,Pia amemshukuru Rais wa Tanzania Mhe Dokta Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha nyingi kwaajili ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo Wilayani hapa.

Akizungumza juu ya bajeti Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Ndg. Michael J.Gwimile amesema kuwa amepokea ushauri na maoni kutoka kwa wajumbe mbalimbali wa baraza la ushauriWilaya  na kusema kuwa wataalam wataendelea kufanya marekebisho  katika bajeti kulingana na maoni na ushauri ulivyotolewa  .

Pia katika suala la ujenzi wa vituo vya Polisi Gwimile ameshauri wananchi wahamasishwe kuchangia  ujenzi vituo vya polisi kama ambavyo wanafanya katika miradi mingine ya maendeleo kwani suala la usalama ni muhimu kwa mustakabali wa Kilosa nzima pia ameongeza kuwa halmashauri inaweza kuongeza nguvu kwa kutenga bajeti kutoka mapato ya ndani ili kumalizia ujenzi wa vituo vya polisi ili kuendelea kuimarisha hali ya ulinzi na usalama kwa wananchi na mali zao.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa