• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

DC SHAKA AWATAKA WANANCHI KUTOJICHUKULIA HATUA MKONONI

Posted on: December 21st, 2023

Wananchi ya Kijiji cha Maguha wamemuomba mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka kutatua kero zao ikiwepo migogoro ya mashamba pamoja kumaliza mipasuko iliyoko baina ya viongozi wa Kijiji na wajumbe wa kamati ya Halmashauri ya kijiji hicho.

Wameyasema hayo katika mkutano ulioandaliwa na mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka ikiwa na lengo la kusikiliza kero za wananchi ambao umefanyika Disemba 20, 2023 katika Kijiji ch Maguha ambapo mkuu wa Wilaya ameambata na vyombo vya ulinzi na usalama na kamati kuu ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kilosa.

Wakiongea kwa nyakati tofauti, wanakijiji wameainisha kuwa baadhi ya miradi ya maendeleo kama vile Zahanati ya Kijiji na Shule ya Msingi Maguha miundombinu yake haijakamilika ikiwemo miundombinu ya umeme katika Zahanati hiyo.

Aidha kero nyingine iliyoainishwa ni wizi wa mali za serikali yakiwemo mabati lakini pia suala la migogoro ya wakulima na wafugaji ilitajwa kuwa ni kero ya muda mrefu.

Kwa upande wa wafugaji wakiwakilishwa na bwana Mnyogi Mhando wameiomba serikali kufikisha huduma ya maji katika makazi yao kwani husafiri kwa umbali mrefu kufuata huduma hiyo lakini pia wamewaomba wakulima kutojuchukua sheria mkononi ikiwa ni pamoja na kuchoma pikipiki zao pale unapotokea mzozo kati ya wakulima na wafugaji.

Hata hivyo, viongozi na wataalamu mbalimbali wakiwemo diwani wa kata ya Maguha bwana Andrea Chaunga, Mtendaji wa Kata ya Maguha bwana Sembuli Mwegalawa, Mtendaji wa kijiji cha Maguha bwana Keneth Mazoba, Mwenyekiti wa Kijiji hicho bwana Fransis Sekwao pamoja na wataalumu kutoka ngazi ya wilaya walipewa nafasi ya kujibu kero zilizowagusa moja kwa moja.

Akitolea ufafanuzi kuhusu utaratibu wa matumizi ya pesa za kiserikali katika akaunti za benki, Mwakilishi wa Mkurugenzi bwana Hussein Ayoub ambaye ni Afisa Utumishi amesema kuwa serikali imeweka utaratibu ambapo fedha hizo hutolewa kwa mfumo wa FAS ambapo Halmashauri ya kijiji hukaa na kupanga matumizi ya fedha zilizopo kisha mkutano mkuu na baada ya hapo hupelekwa kwenye kitengo cha ukaguzi na fedha cha halmashauri ya wilaya ili kuwekewa vifungu vya matumizi ya fedha hizo.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kilosa bwana Shabani Mdoe amewataka viongozi wa serikali ya kijiji hasa wajumbe wa halmashauri ya kijiji kujiepusha na vitendo vya rushwa na kuwataka waoneshe ushirikiano kwa watendaji wa serikali  ili kuleta maendeleo ya kijiji hicho kama Ilani ya chama hicho unavyotaka.

Akiitimisha mkutano huo Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe Shaka Hamdu Shaka amewataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mkoni bali wafuate taratibu za kisheria ili kupata haki yao. Ameongeza kuwa serikali haitasita kumchukulia hatua za kisheria mwananchi yeyote atakayejihusisha na vitendo vya uvunjifu wa amani.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa