• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

DC SHAKA AZITAKA MAHAKAMA WILAYANI KILOSA KUTENDA HAKI KWA WANANCHI

Posted on: February 3rd, 2024

Waheshimiwa Mahakimu wa Mahakama za Wilaya ya Kilosa wametakiwa kutenda haki pindi wanapotoa uwamuzi katika masahauri ya kesi mbalimbali ili kulinda na kusimamia utawala wa kisheria ikiwemo kuondoa migogoro kwa wananchi bila ubaguzi wowote.

Kauli hiyo imetolewa Februari Mosi, 2024 na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka wakati akitoa hotuba yake katika maadhimisho ya sheria nchini yaliyofanyika katika ukumbi wa Mahakama ya Wilayani hapo.

DC shaka amesema kuwa ofisi yake imekuwa ikipokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi wakidai kutotendewa haki katika maamuzi yanayotolewa katika mahakama hizo na kupelekea ofisi yake kuanza kusikiliza kero hizo ambapo amewataka mahakimu hao kuzingatia kauli mbiu yam waka huu isemayo “Umuhimu wa dhana ya haki kwa ustawi wa taifa nafasi ya mahakama na wadau katika kuboresha mfumo junuishi wa haki jinai”.

Ameongeza kuwa Mahakama ni muhimili katika serikali hivyo wanapaswa kushirikiana na wadau wa sheria kutekeleza dhana ya kauli mbiu hiyo kwa kuwajibika, kufanya kazi kwa weledi na uaminifu mkubwa ili kujiepusha na rushwa na mwenendo ambao sio wa maadili kwani changamoto za kesi za migogoro ya ardhi  kwa  wakulima na wafugaji zimekuwa hazitendewi haki .

Aidha amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuhasisi dhana ya haki jinai hivyo wadau wa sheria na vyombo mbalimbali vya ulinzi na usalama waendelee kutekeleza majukumu yao kwa kusimamia haki.

Naye Hakimu Mkazi Mfawidhi katika Mahakama ya Wilaya ya Kilosa Agnes Ringo amesema tangu kuadhimishwa kwa maadhimisho hayo mwaka 1966 yamekuwa chachu kwa maboresho ya mahakama na wananchi ambapo kabla ya kufikia kilele cha maadhimisho hayo mahakama iliweza kutoa elimu ya kisheria maeneo mbalimbali kuanzia tarehe 24 hadi 30 Januari, 2024.

Amesema Mahakama ya Tanzania ina jukumu ya haki kwa watu wote pasipo ubaguzi ambapo katika utekeleza kwa vitendo imekuwa ikifanya maboresho katika utendaji kazi wake ambapo Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua umuhimu huo Januari,2023 aliteua tume ya haki jinai ikitoa pendekezo la kuboreshwa kwa mahakama na wadau katika haki jinai ili haki ionekane imetendeka kwa wakati.

Sambamba na hayo Mhe. Ringo ameongeza kuwa katika kuhakikisha nchi inakuwa na amani mahakama na wadau wana umuhimu kushirikiana katika mfumo jumuishi wa haki jinai kwani maendeleo ya taifa yanategemea uwepo wa amani.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa