• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

DHANA YA USIMAMIZI SHIRIKISHI WA MISITU IWE ENDELEVU

Posted on: June 18th, 2021

Misitu ni rasilimali muhimu kwa maendeleo ya nchi ambayo inahitaji ushirikiano wa kutosha katika kuhakikisha inakuwa endelevu hivyo ipo haja  ya jamii kushirikishwa kwa kiasi kikubwa ili kuhakikisha inatunzwa na kutumika katika hali uendelevu ili kuleta matokeo chanya.

Hayo yamebainishwa na Meneja mradi wa TTCS Bw. Charles Leonard ambapo amesema Tanzania ina hekta 48.1 za misitu hivyo ni vema ikatumika nguvu ya ziada kwa jamii katika kuielemisha na kujenga uelewa namna ya kuhifadhi, kutunza na kutumia misitu katika hali ya uendelevu kwani jamii ikielimika na kupata uelewa mtazamo wao utabadilika kuhusu kulinda, kutunza na kutumia rasilimali misitu.

Leonard amesema kuwa misitu inaweza ikawa endelevu endapo jamii itashiriki kwa kulinda misitu dhidi ya shughuli haribifu za kibinadamu, na kwamba usimamizi shirikishi ni fursa ya maendeleo endelevu ambayo inapunguza uharibifu wa misitu lakini pia inaongeza motisha kwa wananchi na vijiji, Serikali na Halmashauri zinafaidika kwa kupata mapato hivyo ni vema kuendelea kutanua wigo wa kutunza misitu katika njia shirikishi.  

Aidha kwa upande wa Maafisa Habari na Mawasiliano kutoka serikalini na mashirika yasiyo ya kiserikali walioshiriki ziara ya kujenga uelewa juu ya mradi wa Kuleta Mageuzi katika Sekta ya Mkaa Tanzania (TTCS) wamesema mradi huo umetekeleza dhana ya uendelevu wa misitu ya vijiji na kulinda mazingira ambapo mkoani Morogoro unatekelezwa katika wilaya za Kilosa, Mvomero na Morogoro katika vijiji 35 huku wakisema kuwa ipo haja ya mradi huo kufanyika na kuendelezwa nchi nzima kwani una manufaa kwa nchi na wananchi kiujumla.

Pamoja na hayo wamesema mradi huo unachochea utunzwaji wa mazingira na kuinua kipato cha wananchi huku wakisema kuwa endapo Serikali kwakushirikiana na wananchi watatunza misitu hiyo itasaidia katika miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa nyumba za watumishi, ujenzi wa vituo vya afya na zahanati, upatikanaji wa madawati na mbao kwa matumizi mbalimbali jambo litakalosaidia kuepusha matumizi makubwa ya fedha kwa ajili ya ununuzi wa rasilimali za misitu kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

 

Akitoa taarifa fupi ya faida ya mradi wa Mkaa endelevu katika kijiji cha Kitunduweta Afisa Mtendaji wa Kijiji Bw.Thomas Lukoo amesema, “Kijiji cha Kitunduweta kwa mwaka kinavuna vitalu 83 sawa na gunia 6,640 ambapo kwa mwaka wa kwanza walipata Tsh. 28,328,095/=, mwaka 2018/2019 walipata Tsh. 27,128,095/= na mwaka 2019/2020 Tsh. 28,143,255/= lakini wameweza kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo kama kuwakatia wananchi Bima ya Afya ya CHF takribani kaya 378, pia wamefanya ukarabati wa madarasa ya shule ya msingi Kitunduweta, wamemalizia nyumba ya mwalimu mkuu pamoja na kujenga choo cha kisasa cha nyumba ya mwalimu na pia wametengeneza madawati kwa ajili ya shule yao.

Naye Mratibu wa Mradi wa Mkaa Endelevu upande wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa ambaye pia ni Afisa Maliasili Bw. John Mtimbanjayi amesema yapo mafanikio yaliyopatikana baada ya mpango wa usimamizi shirikishi ikiwemo kupungua kwa hali ya uharibifu wa misitu kwa kiasi kikubwa kwani vijiji vinapata fursa ya kupata uelewa namna ya kutunza misitu hiyo lakini pia vinapata fedha zitokanazo na ushuru wa mazao ya misitu, fedha ambazo zinasaidia shughuli za maendeleo kwenye vijiji husika huku akieleza changamoto inayojitokeza kutokana na uwepo wa kanuni ya mapendekezo ya bei ya mazao ya misitu GN417 hususani katika zao la mkaa kuwa na bei  ilekezi ya shilingi 12500 kwa gunia la kilo 50 ambapo awali ilikuwa 6750 hivyo kupelekea wateja wengi kununua mkaa maeneo ya mijini badala ya kununua maeneo ya vijijini ili kuepuka gharama za usafirishaji.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa