• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MIAKA 60 YA UHURU NA 59 YA JAMHURI KUADHIMISHWA KWA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA MAENEO YOTE-DC KILOSA

Posted on: November 24th, 2021

Kilosa yaadhimisha miaka 60 ya Uhuru wa Tanganyika na 59 ya Jamhuri kwa kuishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kiasi cha fedha shilingi bilioni 4.3  zilizotolewa na Serikali ili kuwaletea maendeleo wananchi sambamba na kuendelea kutatua changamoto ya maji kwa kuboresha hali ya upatikanaji wa maji.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mh. Majid H. Mwanga wakati wa maadhimisgho hayo kiwilaya ambapo amesema Serikali imeitupia jicho la tatu Wilaya ya Kilosa kwa kiasi hicho cha fedha ambazo zinawezesha ujenzi wa vyumba 186 vya madarasa kwa shule za sekondari na shule shikizi kwa elimu msingi, ununuzi wa mashine ya mionzi, vyumba vya wagonjwa mahututi na nyumba za watumishi.

Akizungumzia suala la usafi wa mazingira Mwanga amesema katika kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru na 59 ya Jamhuri kila mmoja aadhimishe kwa kufanya usafi katika eneo lake la makazi, biashara na ofisi lengo ikiwa ni kuifanya Kilosa kuwa katika muonekano safi na kwamba Mkuu wa Wilaya atatembelea maeneo mbalimbali ili kukagua na yeyote ambaye hatotimiza agizo hilo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake huku akisisitiza suala la kufanya mazoezi kwa ajili ya kuboresha afya ambapo amesema kwa upande wa Kilosa mazoezi hufanyika kila siku za Jumamosi na Jumapili asubuhi, hivyo anawakaribisha wananchi wote kushiriki mazoezi hayo.

Kwa upande wake Katibu wa CCM Wilaya Shaban Mdoe amepongeza wajasiriamali walioshiriki katika maadhimisho hayo kwa kuonyesha bidhaa wanazofanya ambapo pia amesisitiza urejeshwaji wa mikopo kwa wakati ili vikundi vingine viweze kukopa huku akitoa rai kwa wananchi kuunga mkono juhudi mbalimbali zinazofanywa Serikali ili kuipa Kilosa maendeleo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Kisena Mabuba ameshukuru Serikali kwa namna inavyowaletea maendeleo wananchi ambapo amesema kwa sasa ujenzi wa vyumba vya madarasa unaendelea vizuri katika kata mbalimbali ambapo pia amepongeza wanafunzi walioshiriki katika mashindano ya uandishi wa insha kwa shule za msingi na sekondari ikiwa ni sehemu ya kuchagiza maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru na 59 ya Jamhuri.

Wilaya ya Kilosa imefanya maadhimisho hayo kwa kuendelea kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha jamii kushiriki shughuli za maendeleo katika maeneo mbalimbali, kuwashindanisha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari katika mashindano ya uandishi wa insha na wajasiriamali kuonyesha bidhaa zao ambapo washindi walitangazwa na kupongezwa kwa juhudi zao walizozionyesha.


Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Kilosa kufanya sensa ya mifugo

    December 29, 2022
  • Kilosa kunufaika na mradi wa BOOST

    December 24, 2022
  • Kilosa yaendelea kutambua juhudi za Serikali kwa Watumishi wa Umma na Wananchi-DED Kilosa

    December 19, 2022
  • -Serikali haitosita kulinda Rasilimali watu kwa maslahi ya Maendeleo ya Taifa- Mh. Mhagama

    December 20, 2022
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa