• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

ELIMU IMETOLEWA JUU YA UMUHIMU WA LISHE BORA WILAYANI KILOSA

Posted on: October 31st, 2023

Katika kuadhimisha siku ya Lishe Kitaifa na Uzinduzi wa Kampeni ya Lishe kwa Vijana balehe Elimu imetolewa kwa Jamii juu ya umuhimu wa lishe bora kwa kuzingatia ulaji wa makundi matano ya chakula kwa watoto kuanzia umri wa miezi sita hadi rika balehe itakayosaidia katika ukuaji wao na kuepuka magonjwa yasiyo ya lazima kama vile utapiamlo mkali na udumavu.

Maadhimisho hayo yamefanyika  Oktoba 30, 2023 katika Ofisi ya Kijiji cha Ilonga Wilayani Kilosa ambapo mgeni rasmi akiwa Katibu Tawala wa Wilaya Bi. Salome Mkinga ambaye alimwakilisha  Mkuu wa Wilaya  ya Kilosa.


 Amesema kuwa wazazi na walezi kwa ujumla ni jukumu lao kuzingatia na kuhakikisha watoto wanapata lishe bora ambayo itawafanya wakue vema na kuongeza utendaji kazi wa akili na uwezo wao kitaaluma samabamba na ubunifu wanapokuwa darasani.

Aidha Bi. Mkinga ameongeza kuwa Serikali kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali inatekeleza Mwongozo wa Kitaifa wa utoaji huduma ya Chakula na Lishe shuleni ambao unalenga katika kuhakikisha kila mwanafunzi anapata angalau mlo mmoja akiwa shuleni na kuwajengea wanafunzi uelewa wanapokuwa katika masomo yao.

Naye Afisa Lishe wa Wilaya Bi. Zaina Kibona amewataka wazazi hasa wakiume kutoa ushirikiano wao katika kufatilia hatua za ukuaji wa watoto kwa kuzingatia lishe bora kwa ajili ya afya zao na kutowaachia akina mama peke yao.

Ameongeza kuwa juhudi mbalimbali zimeendelea kufanyika katika kuimarisha afya na ustawi wa vijana balehe kwa kuweka vipaumbele kwenye maeneo yanayolenga kutoa matokea chanya na ya  haraka kwa vijana ikiwemo lishe.

Kwa upande wake Afisa Kilimo wa Kijiji cha Ilonga Bi. Martha Kulewa ametoa wito kwa jamii juu ya upandaji wa bustani za mbogamboga kwa kutumia viroba ambapo haitaji eneo kubwa la shamba ili kurahisisha upatikani wa lishe bora kwa watoto kwa ajili ya ustawi wa afya zao na kuimarisha ukuaji na kuondoa udumavu na utapiamlo.

Maadhimisho ya siku ya lishe kitaifa  yanalenga kuimarisha Juhudi zilizopo nchini na yatajumuisha uzinduzi wa kampeni ya lishe kwa vijana balehe  ambayo kauli mbiu ya maadhimisho  2023 “ Lishe bora kwa Vijana Balehe, Chachu ya Mafaniko yao”.

 

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa