• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

ELIMU YA MALISHO YA MIFUGO IPELEKWE SEHEMU HUSIKA

Posted on: December 11th, 2018

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Abdallah Ulega amekiagiza Chuo cha Mifugo LITA Morogoro kuhakikisha kinawaleta wanachuo  kwa mafunzo kwa vitendo katika maeneo husika hasa ya wafugaji badala ya kuwapeleka katika mafunzo kwa vitendo maeneo ya mijini yasiyo na jamii ya wafugaji kwani wakiwapeleka maeneo husika itasadia kuifanya kazi yao kwa vitendo lakini pia itawasaidia jamii husika hasa ya wafugaji kupata elimu namna ya kuandaa malisho ya mifugo yao.

Ulega amesema hayo alipokuwa katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Kata ya Parakuyo ambapo amesema chuo hicho kinapasa kuwaleta wataalam katika maeneo ya ufugaji ili kuwasaidia wafugaji kuandaa namna bora ya kuandaa malisho kwa ajili ya mifugo hasa kipindi cha kiangazi kunapokuwa na uhaba wa malisho jambo ambalo husababisha wafugaji kuhama hama kwa ajili ya kutafuta malisho ambapo husababisha kutokea kwa migogoro ya wakulima na wafugaji.

Naye mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi amemshukuru Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi kwa ziara yake ambapo ameagiza ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na meneja wa Lanchi ya Mkata kuyafanyia kazi maagizo yaliyotolewa dhidi ya wawekezaji wasioendeleza maeneo wanayoyahodhi sambamba na wawekezaji waliokodisha maeneo ya lanchi kwa ajili ya kulima.

Aidha Mgoyi ametoa wito kwa wafugaji kuwa wakweli kuhusiana na idadi ya mifugo waliyonayo kwani kitendo cha kuwa wakweli kitasaidia wilaya kupanga mipango yake kwa usahihi na kwamba kwasasa baadhi ya wafugaji wameanza kuitumia vyema elimu ya ufugaji wa kisasa waliyopewa na kwamba ofisi yake inategemea wafugaji hao wataendelea kutoa ushirikiano wa kutosha ili kuijenga Kilosa Mpya.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kilosa Ameir Mbarak amesisitiza kufanyika ka tahmini ya kina kutambua mipaka kwa maeneo ya wilaya ili kuepuka migogoro ya mipaka na uvamizi wa maeneo ama kutumika kwa maeneo kinyume na taratibu na kwamba kila mtu aheshimu maeneo hayo na kuyatumia kwa kufuata taratibu na sheria.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa