• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA YATOA MIKOPO KWA MAKUNDI MAALUM

Posted on: February 21st, 2020

Halmashauri ya Wilaya  ya Kilosa imekabidhi hundi ya kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 110 kwa vikundi 12 ambayo ni mkopo kwa makundi  ya Wanawake , Vijana na walemavu  ikiwa ni asilimia kumi ya makusanyo ya mapato ya ndani kwa kipindi cha mwaka wa fedha mwezi Oktoba hadi Disemba 2019/2020 .

  

Hundi hiyo imekabidhiwa FebruarI 21 mwaka huu katika ukumbi wa halmashauri na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adamu Iddi mgoyi ambaye alikuwa mgeni rasmi amesema kuwa anamshukuru Mkurugenzi  na Halmashauri yake kwa ujumla kwa kufanya maamuzi magumu kutoa fedha za watu masikini  na kutekeleza sheria ya Serikali kutoa asilimia kumi kwa makundi ya watu maalumu kwa asilimia mia moja. 

MKUU WA WILAYA YA KILOSA ADAM MGOYI

Amesema kuwa Halmashauri kutoa fedha hizo si jambo jepesi  kwasababu maagizo na maelekezo mengi ambayo Halmashauri wanayapata kutoka Serikali Kuu yanazidi asilimia miamoja ya mapato yote ya ndani na kwamba amevitaka vikundi vilivyo chukua fedha hizo wakatekeleze miradi walioombea mkopo na si vinginevyo,  kwani fedha hiyo ni ya mkopo  na inahitajika kurejeshwa kwa wakati ili watu wengine waweze kukopeshwa.

Mgoyi  amesema  vikundi hivyo  lazima  viwe na umiliki wa mradi kila mtu ashiriki na kufuatilia mwenendo wa mradi na  sio kumuachia mtu mmoja kusimamia kwani  ni muhimu kila mwana kikundi kushiriki katika vikao na kusomewa mapato na matumizi kwa mujibu wa taratibu zao za vikao na kwamba watambue kuwa Serikali ina mpango madhubuti wa kuwainua wananchi wake ili waondokane na umasikini hivyo fedha hizo hazitolewi kama zawadi  bali zinatolewa kwa mkopo na kufanyiwa ufuatiliji ili ziweze kusaidia  kuwaondoa katika umasikini kwani fedha hizo  zikitumika kinyume na makusudio ya mkopo watapata hasara na kuishia pabaya.

KAIMU MKURUGENZI WA HALMASHAURI BW. NKELEGE (ALIYESIMAMA MWENYE SHATI LA KITENGE)

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa  Halmashauri ya Wilaya Kilosa Cheyo  Nkelege amesema kuwa Halmashauri imeweza kutenga asilimia 10 kwa makusanyo ya mapato ya ndani na kwamba Wilaya ya Kilosa ni kubwa na ina vikundi vingi,  hivyo amewapongeza wale waliokidhi vigezo kupewa fedha hizo  na kwamba  amevitaka vikundi vikasimamie vizuri ili waweze kufikia malengo walio kusudia huku akiahidi kuwa Halmashauri itavifikia vikundi vyote vilivyo kidhi vigezo na kuvikopesha .

Akisoma taarifa ya kukabidhi hundi hiyo Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya Simforosa Mollel amesema kuwa Halmashauri imeendelea kutekeleza takwa la kisheria la kutoa mikopo ya makundi maalumu ambapo katika kipindi cha mwezi Oktoba hadi Disemba 2019/2020  Halmashauri imeweza kutoa fedha kwa mifuko ya maendeleo ya wanawake ,Vijana na watu wenye ulemavu kiasi cha shilingi milioni mia moja na kumi , lakitano ishirini na tisa ,mia mbili ishirini na tisa senti sita tisa(110,529,226.69) zimeidhinishwa kutolewa ili walengwa wenye sifa waweze kupata mikopo hiyo kama ilivyoainishwa katika sheria ya fedha ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1982 na marekebisho yake ya mwaka 2018 huku akisema kuwa  jumla ya vikundi kumi na mbili [12] vimeidhinishiwa mkopo ambapo vikundi vya wanawake vimepata kiasi cha shilingi milioni 44,211690.68,  vijana 44,211690.68 na watu wenye ulemavu Tsh 22 105845.33.

MAKAMU MWENYEKITI WA HALMASHAURI MH. HASSAN KAMBENGA AKIWA NI MOJA KATI YA WALIOSHUHUDIA ZOEZI HILO LA KUKABIDHI HUNDI

Nao wana vikundi wameishukuru Halmashauri kwa ujumla kwa  kuwaamini kwani  jamii imekuwa na mtazamo hasi kwa vijana kuwa hawaaminiki na kwamba wameihakikishia Halmashauri kuwa fedha waliyokopeshwa  itakwenda kufanya kazi iliyokusudiwa na kuzirejesha kwa muda muafaka ili ziweze kusaidia na wengine.

BAADHI YA WANAVIKUNDI WALIOKABIDHIWA MKOPO NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa