• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

HALI KIBIASHARA IKO CHINI - DC

Posted on: December 20th, 2018

Imebainika kuwa hali ya kibiashara wilayani Kilosa iko chini ya mstari wa umaskini ambapo wastani wa pato la mtu ni shilingi 750 kwa siku hali inayoashiria mzunguko wa kuuza na kununua uko chini unaopelekea pato la wilaya kuwa chini sana licha ya kuwepo kwa fursa mbalimbali zilizopo wilayani ambazo hakuna mtu anayezifanyia kazi.

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi amebanisha haa wakati wa kikao cha Baraza la Biashara Wilaya ambapo amesema kuwa pamoja na kuzalisha mazao ya kilimo yanazalishwa lakini yanauza yakiwa hayapo katika mnyororo wa thamani ili kuongeza tija halkadhalika upande wa mifugo kwa asilimia kubwa hali bado ni duni kwani fursa za mifugo zipo ikiwemo biashara za ngozi lakini hakuna anayeshiriki ili kujiongezea kipato.

Aidha Mgoyi ametoa rai kwa TCCIA NA Jumuia ya wafanya biashara(JWT) kujiunga katika vikundi vitakavyosaidia kuwa na viwanda vidovidogo vitakavyosaidia kupata tija na kuongeza kipato kwani fursa za kuwa na viwanda vya aina mbalimbali zipo ikiwamo uanzishwaji wa viwanda kama vya sabuni ambapo malighafi zote zinapatikana hapa hapa wilayani badala ya kuagiza toka nje sambamba na kuitazama fursa uwepo wa reli ya standard gauge kuwa ni fursa adhimu kwani inaweza kutengeneza ajira kwa kuwa wabunifu na kuibua biashara za aina mbalimbali kwani kupitia standard gauge upo uwezekanao mkubwa kuongeza kipato bila kusahau kulipo kodi na tozo stahiki kwa mujibu wa sheria na taratibu.

Aidha katika kikao hicho Katibu wa Kamati ya Uwekezaji Wilaya Karoli Leonce akiwasilisha fursa za uwekezaji na hali ya uanzishaji viwanda vipya ndani ya wilaya kwa kipindi cha 2018 ili kufikia azma ya upatikanaji wa viwanda 37 wilayani ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la kuwa na viwanda ambapo amesema katika sekta ya kilimo uwekezaji unaweza kufanyika katika mazao ya pamba, karanga, alizeti, tumbaku, miwa, mahindi,mbogamboga pamoja na ujenzi wa maghala, huku sekta ya mifugo kukiwa na upatikanaji wa nyama na ngozi, sekta ya elimu ikiwa katika ujenzi wa shule binafsi, nishati upande wa uzalishaji umeme, sekta ya mazingira upande wa usafi na mazingira, sekta ya utalii,sekta ya ardhi ukodishaji wa nyumba

Naye Kaimu Afisa Mipango Wilaya Lwomile Vallence amesema kuwa mpango mkakati wa Baraza la Biashara Wilaya chini ya kaulimbiu uchumi wa viwanda na maisha bora ni kuboresha huduma kwa wateja kwa kuhakikisha 80% ya wafanyabiashara wawekezaji wanaridhika na huduma zitolewazo ifikapo Juni 2020, kuhamasisha uwekezaji wa viwanda ndani ya wilaya ambao utaongeza makusanyo kwa mwaka kufikia 5,000,000 ifikapo Juni 2020 pamoja na kufanya mabadiliko katika sekta ya kilimo na mifugo kwa kuhakikisha zaidi ya 50% ya wakulima na wafugaji wa ndani ya Wilaya wanalima na kufuga kibiashara, tija na masoko ya uhakika ifikapo Juni 2020.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kikundi cha Mary’s kinachojihusisha na usindikaji wa mazao ya mboga mboga, matunda na nafaka Bi Marygrace Ng’unga amesema kuwa ili kuweza kufikia uchumi wa viwanda na maisha bora ipo haja kwa Halmashauri kusaidia kutatua changamoto ya upatikanaji wa vifungashio, mchakato wa kupata nembo ya ubora ya TBS, TFDA pamoja na uwezeshaji wa kifedha.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa