• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

HALMASHAURI AMBAZO HAZIMALIZA UJENZI ZAHIMIZWA KUMALIZA

Posted on: December 17th, 2021

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI David Silinde ameagiza uongozi wa Halmashauri za Wilaya katika mkoa wa Morogoro ambazo bado wapo nyuma katika ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa kuhakikisha wanasimamia kwa karibu zaidi mafundi ili waweze kukamilisha kwa wakati katika muda ulioongezwa na Serikali ifikapo Disemba 30, 2021 ili kuruhusu wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza kuanza kutumia madarasa hayo.

Ametoa maagizo hayo wakati akikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika halmashauri nne za mkoa wa Morogoro ambazo ni Gairo, Kilosa, Mvomero na Manispaa ya Morogoro na kukuta ni halmashauri moja tu ya Kilosa ndiyo iliyomaliza ujenzi kwa asilimia mia huku halmashauri ya Gairo ikiwa bado ipo nyuma wakiwa wanaezeka mabati katika majengo yao yote waliyopewa na kutaka waongeze spidi kwa kufanya kazi usiku na mchana kwani muda ulioongezwa ni mdogo kuliko kazi ambazo bado wapo nazo.

Ameongeza kuwa ametembelea halmashauri ambazo zipo mbali sana na viwanda vya saruji zinapozalishwa na vifaa vingine kama Katavi, Rukwa, Songwe lakini wamekamilisha majengo yao lakini inashangaza kuona mkoa wa Morogoro ambao upo karibu na viwanda vya uzalishaji wa vifaa bado upo nyuma kukamilisha kwa uharaka ujenzi wa madarasa na kutaka wakamilishe kwa wakati ikiwezekana kabla ya tarehe ya mwisho kwa ubora na thamani halisi ya fedha ionekane.

Kwa upande wake Katibu Tawala mkoa wa Morogoro Mariam Mtunguja amesema sababu kubwa ya halmashauri ya Gairo kuwa nyuma katika ujenzi wa madarasa ni kutokana na kuagiza saruji Tanga ambapo walikuta foleni kubwa ya uhitaji wa bidhaa hivyo kuchelewa lakini wanaamini ndani ya muda ulioongezwa watakamilisha kwa wakati na halmashauri zingine ambazo zinakamilisha ujenzi huo.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro Pascal Kihanga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa vyumba vya madarasa ambavyo sasa vitasaidia kupunguza mrundikano wa wanafunzi katika chumba kimoja ambao walikua wanawaweka mpaka wanafunzi 100 kwa wakati mmoja lakini sasa watakaa wanafunzi 45 tu hivyo kufanya ufaulu kuongezeka. 

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa