• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

HALMASHAURI AMBAZO HAZIMALIZA UJENZI ZAHIMIZWA KUMALIZA

Posted on: December 17th, 2021

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI David Silinde ameagiza uongozi wa Halmashauri za Wilaya katika mkoa wa Morogoro ambazo bado wapo nyuma katika ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa kuhakikisha wanasimamia kwa karibu zaidi mafundi ili waweze kukamilisha kwa wakati katika muda ulioongezwa na Serikali ifikapo Disemba 30, 2021 ili kuruhusu wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza kuanza kutumia madarasa hayo.

Ametoa maagizo hayo wakati akikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika halmashauri nne za mkoa wa Morogoro ambazo ni Gairo, Kilosa, Mvomero na Manispaa ya Morogoro na kukuta ni halmashauri moja tu ya Kilosa ndiyo iliyomaliza ujenzi kwa asilimia mia huku halmashauri ya Gairo ikiwa bado ipo nyuma wakiwa wanaezeka mabati katika majengo yao yote waliyopewa na kutaka waongeze spidi kwa kufanya kazi usiku na mchana kwani muda ulioongezwa ni mdogo kuliko kazi ambazo bado wapo nazo.

Ameongeza kuwa ametembelea halmashauri ambazo zipo mbali sana na viwanda vya saruji zinapozalishwa na vifaa vingine kama Katavi, Rukwa, Songwe lakini wamekamilisha majengo yao lakini inashangaza kuona mkoa wa Morogoro ambao upo karibu na viwanda vya uzalishaji wa vifaa bado upo nyuma kukamilisha kwa uharaka ujenzi wa madarasa na kutaka wakamilishe kwa wakati ikiwezekana kabla ya tarehe ya mwisho kwa ubora na thamani halisi ya fedha ionekane.

Kwa upande wake Katibu Tawala mkoa wa Morogoro Mariam Mtunguja amesema sababu kubwa ya halmashauri ya Gairo kuwa nyuma katika ujenzi wa madarasa ni kutokana na kuagiza saruji Tanga ambapo walikuta foleni kubwa ya uhitaji wa bidhaa hivyo kuchelewa lakini wanaamini ndani ya muda ulioongezwa watakamilisha kwa wakati na halmashauri zingine ambazo zinakamilisha ujenzi huo.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro Pascal Kihanga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa vyumba vya madarasa ambavyo sasa vitasaidia kupunguza mrundikano wa wanafunzi katika chumba kimoja ambao walikua wanawaweka mpaka wanafunzi 100 kwa wakati mmoja lakini sasa watakaa wanafunzi 45 tu hivyo kufanya ufaulu kuongezeka. 

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Program ya Dunia Yangu Bora Yawa Chachu Njema Mashuleni

    August 11, 2022
  • Maonesho ya Nane Nane kuwa Endelevu

    August 08, 2022
  • Fanyeni Maonesho ya Nane Nane kuwa na tija - Mh. Pinda

    August 04, 2022
  • RUWASA, MORUWASA shirikianeni na taasisis nyingine kuibua vyanzo vya maji

    August 02, 2022
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu:

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa