• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

HALMASHAURI YAFANIKIWA KUFIKIA MALENGO UTOAJI CHANJO

Posted on: November 15th, 2019

Imeelezwa kuwa zoezi la utoaji wa chanjo ya surua/Rubella katika Wilaya ya Kilosa lililofanyika kuanzia tarehe 17/10/2014 hadi tarehe 21/10/2019 katika vituo 56 vya kutolea huduma ya mama na mtoto wilayani Kilosa sambamba na utoaji chanjo ya Polio ya Sindano katika Halmashauri imefikia malengo katika utoaji wa chanjo hizo kama inavyotakiwa na Muongozo wa Chanjo wa Taifa.

Hayo yameelezwa na Muuguzi mkuu Wilaya Mwanaisha Chitanda  wakati wa utoaji taarifa ya chanjo baada ya kampeni ya kitaifa ambapo amesema kuwa walengwa wa zoezi hilo walikuwa watoto wa umri wa chini miaka mitano kwa upande wa chanjo ya Surua/Rubella miezi 9-59 juku IPV  Miezi 18-42 ambapo usambazaji wa chanjo na vifaa ulifanyika kwa kutumia  timu zilizokwenda kwenye kanda pia zilitumika kutoa mafunzo kwa Watumishi waliokuwepo kwenye kanda hizo.

Chitanda amesema kuwa katika kufanikisha kampeni hizo yapo mafanikio yaliyojitokeza ikiwemo kufanyika kwa kikao cha Kamati ya Huduma ya Afya ya Msingi Wilaya (PHC) ambacho kilifanyika ili kusaidia kufanya uhamasishaji katika ngazi ya jamii juu ya  zoezi la utoaji wa Chanjo ya Surua na Polio ya Sindan, Jumla ya watoa huduma 330 walipewa mafunzo ya utekelezaji zoezi katika kanda 4 (Lumuma, Mikumi, Kilosa Mjini na Dumilapamoja na usimamizi uliofanyika katika vituo vya kutolea chanjo ikiwa ni pamoja na kutatua mapungufu yaliyojitokeza , km chanjo, na vifaa mbalimbali vya kutolea chanjo.

Pamoja na hayo amesema katika zoezi hilo zipo changamoto zilizojitokeza ikiwemo kuchelewa kwa fedha hivyo kufanya kazi ya uratibu wa zoezi hilo kuwa ngumu,  baadhi ya maeneo katika Wilaya kutofikika kwa urahisi kutokana na Changamoto za kijiografia, hususani uwepo mvua nyingi katika maeneo ya Lumbiji, Uleling’ombe, Chonwe, Mbamba, Unone, Vidunda na Munisagara.

Wakati huo huo mradi wa WARIDI unaofikia ukomo wake umetoa taarifa ya Utekelezaji wa mradi wa Usafi wa Mazingira katika Halmashauri ya wilaya – Kilosa mradi ulioanza Agosti 25, 2017  na kutarajiwa kuhitimishwa Disemba 31, 2019 ambapo umefanikiwa katika kuteleta mabadiliko katika maeneo mbalimbali kwa kipindi chote ulipokuwa ukitekelezwa wilayani Kilosa

Akieleza mafanikio hayo mdau toka WARIDI Shadaiya Rwehabula amesema miongoni mwa mafanikio hayo ni kaya zenye vyoo zimeongezeka kutoka kaya  89258(90%) hadi kufikia kaya 105147(97.3%). kaya zenye vyoo bora zimeongezeka kutoka kaya 33675 (35.6%) hadi 53111 (49%), kaya zenye vyoo vya asili zimepungua kutoka asilimia 64.4 na kufikia 51, kupungua kwa kaya zisizo na vyoo kutoka kaya 8717 sawa na asilimia 10 ya kaya zote hadi kufikia kaya 2950 sawa na asilimia 2.7, unawaji mikono umeongezeka kutoka kaya 22916 sawa na asilimia 24 hadi kufikia kaya 42259 sawa na asilimia 39. vijiji 72 sawa na 52% kati ya 139  vimefikia lengo la kaya zote kuwa na vyoo  katika kijiji .

Mafanikio mengine ni vijiji 52 (74%) kati ya 72  vilivyofikia lengo la kila kaya kuwa na choo katika kijiji vimefanya uhakiki wa ndani , vijiji 52(100%) vilivyofanya uhakiki wa ndani wa ujenzi na matumizi ya vyoo vimefanyiwa  uhakiki wa nje na timu ya  Mkoa, Halmashauri na WARIDI,  vijiji 41 vimefanikiwa kupata madaraja ya usafi  vijiji 11 havikufaulu kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo taasisi kutokuwa na vyoo bora, maeneo ya wazi, migahawa, mikusanyiko kutokuwa safi na baadhi ya kaya kuwa na vyoo hafifu sana (mf. Vyoo vya masulphate).

Naye Afisa Afya Wilaya esther Nyabahwera amesema chini ya mradi wa waridi wamejifunza kufanya kazi kama timu katika ngazi zote kwenye uhamasishaji, ufuatiliaji, ukusanyaji wa takwimu, uchukuaji wa hatua za kisheria na maamuzi ya pamoja ili kwenda mbele katika malengo tuliyojiwekea ya kuiweka jamii nzima kuwa na mazingira safi, motisha  kwa wakusanya taarifa za usafi wa mazingira kusaidia kupata taarifa kwa wakati na sahihi, umuhimu wa mafunzo rejea kwa wakusanya takwimu za usafi wa mazingira kwa kila robo pamoja na kuboresha usafi wa mazingira ngazi ya kaya,taasisi na maeneo ya jumuiya.

Akihitimisha uwasilishaji wa taarifa zote mbili ya waridi na chanjo Mganga Mkuu wa Wilaya Dokta Halima Mangiri ametoa wito kwa wadau wa afya kuendelea kutoa ushirikiano hasa katika sekta ya afya ili kuhakikisha wilaya kiujumla inakuwa katika hali ya usafi wa mazingira kwa kuhakikisha tunaendeleza mazuri yote na elimu iliyotolewa na waridi sambamba na kushiriki kikamilifu katika shughuli za afya kama vile hamasa katika chanjo na huduma nyingine zinazotolewa katika sekta ya afya, huku akiahidi kufanyiwa kazi kwa mapendekezo yaliyotolewa na washiriki wa vikao hivyo ili kuboresha huduma za afya na usafi wa mazingira.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA SHULE YA SEKONDARI MASANZE

    May 20, 2025
  • WATENDAJI NGAZI YA HALMASHAURI WATAKIWA KUWA WAADILIFU

    May 14, 2025
  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa