• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Idara ya Ardhi ipewe kipaumbele ili kuingiza mapato - Naibu Waziri - Ardhi

Posted on: September 27th, 2018

Naibu waziri wa Ardhi,  Nyumba na Makazi Mhe. Angelina Mabula amesema kuwa sekta ya ardhi ikiangaliwa kwa jichola karibu na kupewa kipaumbele ni moja ya maeneo ambayo yanaweza kiingizia mapato Serikali  kutokana na shughuli mbalimbali zinazofanyika ndani ya sekta hiyo ikiwemo malipo kwa ajili ya viwanja kwani sekta hiyo ni sekta mama na kwamba asilimia kubwa ya shughuli zote hufanyika kupitia ardhi.

Mabula amesema hayo Septemba 26 alipotembelea Wilaya ya Kilosa kwa ziara ya siku moja na kusema kuwa Idara ya Ardhi ikitelekezwa ni rahisi kuzaa migogoro ya ardhi kutokana na ufanisi wa kuwa chini,  hivyo ni vema wakurugenzi wote nchini kila mmoja katika Halmashauri yake akatilia mkazo suala hili ili kuepuka migogoro ya ardhi ambayo si ya lazima lakini pia kutokuwepo kwa migogoro kutasaidia Halmashauri kuingiza mapato kwa urahisi na kupunguza malalamiko kutoka kwa wananchi tunaopaswa kuwahudumia.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri huyo amatembelea mashamba mbalimbali yakiwemo yaliyo na migogoro kama vile Farm Africa Agrofocus (T) Ltd lenye ukubwa wa ekari 13200.225, mashamba  6 yanayopendekezwa kufutwa Chanzuru yenye ukubwa wa ekari 1598 chini ya mmiliki Sadrudin Rajabal Meghji, mashamba mawili yaliyopo Kimamba shamba lenye ukubwa wa ekari  6945 chini ya mmiliki Sino Development  Company na Sumagro Ltd lenye ukubwa wa ekari 7712 yote yakiwa hayajaendelezwa, pamoja na hayo kiongozi huyo na msafara wake walitembelea mashamba yaliyobatilishwa umiliki na mheshimiwa Rais yenye ukubwa wa ekari 8679 yaliyopo Mvumi na mwisho walitembelea mashamba pori  yaliyotolewa notisi ya mwisho yakiwa Magole yenye ukubwa wa ekari  3507

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi alitumia fursa ya ziara hiyo ya Naibu Waziri kutoa ombi la mapendekezo la mashamba yanayopendekezwa kufutwa kwamba yawezwe kufutwa ili wapewe wawekezaji ambao wako tayari kwa ajili ya uwekezaji na kwamba kwa kufanya hivyo itasaidia kuongeza kipato kwa Halmashauri na kuleta maendeleo kiujumla katika wilaya nzima ikiwemo vijana kupata ajira kupitia uwekezaji utakaofanyika.

Aidha Afisa Mipango Miji na Vijiji Wilaya Masheka Mtatiro amesema Halmashauri inaweza kukusanya mapato kupitia ardhi  kwa kukusanya kodi zote zitokanazo na ardhi kupitia mfumo wa  Land Rent Management System (LRMS) na kupitia mfumo wa Government Electronic  Payment Gateway (GEPG)  makusanyo mengine yanaweza kukusanya kama vile kuhamisha ardhi, kuhuisha ardhi, ada ya upimaji nk.

Akihitimisha ziara yake Naibu Waziri ameitaka Idara ya Ardhi kuandaa taarifa ya kila robo mwaka itakayoonyesha wadaiwa sugu na hatua zilizochukuliwa, pia ametaka viwanja vyote ambavyo havijapimwa viweze kupimwa, uandikishaji wa hatimiliki ufanyike ili kuwasaidia wananchi kuwa na hati  zitakazowasaidia na kuondoa migogoro,  pamoja na kuandaa mpango kabambe  ili ardhi itumike katika mpangilio sambamba na kuwataka watumishi wa Idara ya Ardhi kutokaa ofisini muda mwingi bali wawafikie wananchi na kuwahudumia inavyostahili huku wakishirikiana na Ofisi ya Kanda ili kuwasaidia katika changamoto mbalimbali zinazowakabili ili Kilosa iwe salama dhidi ya migogoro ya ardhi.

 

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 KWA SHULE ZA SEKONDARI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA July 14, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI September 16, 2023
  • ZABUNI January 31, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • KILOSA KUDUMISHA USAFI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    September 20, 2023
  • TIMU YA UKAGUZI MKOA YATEMBELEA MIRADI YA BOOST KILOSA

    September 20, 2023
  • MAPATO YA HALMASHAURI YAONGEZEKA KUTOKA ASILIMIA 94 MPAKA ASILIMIA 98.91

    September 01, 2023
  • Walimu watakiwa kuendelea kuzifahamu huduma za kibenki

    August 29, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa