• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Ijue chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi

Posted on: May 4th, 2018

Imebainika kuwa Saratani ya mlango wa kizazi ambayo husababishwa na virusi vya Human Papilloma ina athari kubwa kwa afya ya wanawake ulimwenguni kote. Inakadiriwa kuwa kila mwaka kati ya wanawake 466,000 wanathibitika kuwa na saratani ya mlango wa kizazi, na wengi wao wako katika nchi zinazoendelea,ikiwemo Tanzania.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi wakati wa uzinduzi wa kampeni ya  Chanjo ya kuzuia Saratani ya Mlango wa kizazi ili kutokomeza maambukizi ya saratani ya mlango wa kizazi kwa mabinti wenye umri wa miaka 14, ambapo amesema kuwa kutokana na ukubwa na ugumu wa kugundua tatizo kwa wananchi walio wengi serikali imeona umuhimu wa kuanzisha chanjo hii ili kulinda kundi kubwa lisipatwe na madhara ya ugonjwa huu wa hususani kwa mabinti hawa wenye umri wa miaka 14, ili kuzuia madhara ya ugonjwa kwao kwani isije ikawa kikwazo katika kufikia malengo yao na ndoto zao.

Miongoni mwa viashiria vya ugonjwa huu ni kuanza kujamiana katika umri mdogo,Kuwa na wapenzi wengi,Kuwa na ndoa za mitala,Kuzaa watoto wengi na Uvutaji sigara,Aidha dalili zake ni Kutokwa damu bila mpangilio au kutokwa na damu baada ya kujamiana,Maumivu ya mgongo, miguu na au kiuno,Kuchoka, kupungua uzito, kupungikiwa hamu ya kula,Kutokwa uchafu uchafu wa majimaji uliopauka wa rangi kahawia au wenye damu kwenye uke na Kuvimba mguu mmoja

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto imeanzisha chanjo ya virusi vya HPV ambayo ni salama, haina madhara na inatolewa bila malipo katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya, shuleni na kwenye vituo vya huduma za mkoba, na ili kupata kinga kamili, binti anatakiwa apate chanjo ya HPV mara mbili. Chanjo ya pili anatakiwa aipate miezi sita baada ya kupata chanjo ya kwanza.

Sambamba na hayo katika tukio hilo la uzinduzi wa chanjo hiyo ya saratani ya mlango wa kizazi iliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Kilosa  Town iliyohudhuriwa na wazazi, walimu, viongozi wa mashirika ya dini pia wananchi walijitokeza kwa wingi ili kupata elimu ya ugonjwa huo pamoja na kuwaleta watoto wao waweze kupata chanjo hiyo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa