• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

ISHINI MAISHA YA MAADILI NA TUNU MLIYOFUNDISHA SHULENI - NW ELIMU

Posted on: September 30th, 2018

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Tate Olenasha amewataka wanafunzi wote nchini wanaomaliza kidato nne pindi wamalizapo elimu hiyo kuishi maisha ya maadili na tunu waliyojifunza shuleni ili kuweza kukubalika katika jamii na kufanikiwa katika maisha yao ya sasa na hapo baadaye.

Olenasha amesema hayo alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 22 ya shule ya Sekondari Msolwa St. Gaspare Bertoni iliyopo kata ya Kisanga wilayani Kilosa ambapo amesema kumekuwa na hulka ya wanafunzi wanapomaliza kidato cha nne kuishi maisha yasiyofaa ya makundi mabaya jambo ambalo halistahili kwani wanafunzi hao wanapokuwa shuleni hufundishwa kuishi kwa maadili ambapo lengo la maadili hayo si kwa kipindi wanachokuwa wanafunzi bali ni kwa ajili ya maisha yao yote ili waweze kufanikiwa.

Olenasha ameongeza kusema kuwa serikali iko bega kwa bega na sekta binafsi hasa katika sekta ya elimu kwa kutoa ushirikiano ili kuhakikisha elimu na mafunzo yanayotolewa na sekta binafsi yanaendana na sera za awamu ya tano za kuwa na elimu bora itakayozaa wataalam wazuri na wasomi wenye kukidhi viwango vitakavyosaidia serikali ya Tanzania kiujumla.

‘‘Aidha niseme kuwa serikali ya awamu ya tano inatambua uwepo wa shule za binafsi na inaunga mkono juhudi zinazofanywa na sekta binafsi hasa upande wa elimu kwa kuweka mazingira wezeshi ili wawekezaji katika sekta ya elimu wawekeze katika mazingira mazuri pamoja na ushirikiano ili kupata watumishi wazuri wenye kuisaidia serikali na kuleta maendeleo’’ Ameongeza Olenasha.

Akieleza mafanikio yanayotokana na mpango wa elimu bure bila malipo amesema kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi waliojiandikisha elimu ya msingi, ujenzi wa shule umeongezeka kutokana na uhitaji kuwa mkubwa,  ongezeko la vitendea kazi kutokana na kuongezeka kwa wanafunzi, mikopo imeendelea kutolewa kwa wanafunzi wa elimu ya juu pamoja na waratibu elimu kata nchini kupatiwa pikipiki ili kurahisisha utendaji kazi na ufatiliaji wa maendeleo ya elimu kwa wanafunzi.

Akisoma risala kwa mgeni rasmi Mkurugenzi wa shule hiyo Bw. Godfrey Kolowoga amesema licha ya shule hiyo kuendana na changamoto za ukuaji wa sayansi na teknolojia hususani TEHAMA shule hiyo imefanikiwa kuwa na tovuti kwa lengo la kurahisisha mawasiliano na kupeana habari katika ulimwengu wa utandawazi,  lakini pia inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo miundombinu ya usafiri, uchache wa vyumba vya maabara kwa ajili ya mazoezi kwa vitendo kwa masomo ya sayansi kwani haiwekani kuwa na wanasayansi wazuri wa baadaye pasipokuwa na maabara.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa