• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

JAMII WILAYANI KILOSA YATAKIWA KUZINGATIA MWONGOZO WA CHAKULA NA ULAJI

Posted on: October 30th, 2024

Jamii  Wilayani Kilosa imetakiwa kuzingatia  mwongozo wa Kitaifa wa chakula na ulaji ,ili kuondoa dhana potofu na mitizamo hasi iliyopo juu ya ulaji na ulishaji watoto ili kujenga familia yenye ustawi na afya njema.

Hayo yameelezwa Oktoba 30,2024 na Kaimu Afisa Lishe Wilaya ya Kilosa Elisha Kingu wakati wa maadhimisho ya Siku ya Lishe Kitaifa ambapo Kiwilaya yamefanyika katika kata ya Msowero kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Msowero.

Kingu amesema kuwa lengo la maadhimisho hayo ni kuendelea kujengeana uwezo kuhusu masuala ya lishe na chakula kwa kufuata muongozo wa Taifa wa chakula na kwamba kuna makundi 6 ya chakula  na yote yanapatikana katika maeneo mbalimbali wilayani hapa  hivyo ameisisitiza jamii kula kwa kuzingatia makundi hayo angalau kila mlo uwe na kundi moja au mawili ya chakula.

Amesema kula kwa kuzingatia makundi hayo ya chakula kunasaidia kujikinga dhidi ya magonjwa lakini pia jamii itakuwa na nguvu ya kutimiza wajibu huku ikisaidia kumjenga mtoto akuwe katika hali nzuri,arefuke na kuwa na uzito unaofaa huku ufahamu wake ukiwa katika hali inayostahili hivyo kumuwezesha kufanya vizuri katika masomo.

Sambamba na hayo amesema kuwa ni muhimu kwa Mama mjamzito na familia nzima kwa ujumla kuhakikisha  inapata chakula kinachokidhi mahitaji ya mwili ,huku akisistiza familia kuzingatia kutumia vyakula vyenye virutubisho vilivyoongezwa ikiwemo madini pamoja na Vitamini ili kupata virutubisho vya ziada na kujenga jamii yenye afya bora hivyo kuzalisha watu wenye uelewa mzuri kwa faida ya Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Afisa Afya Mbaraka Lilanga amewataka wananchi kutumia maji safi na salama kwaajili ya kunywa pia amewasisitiza kuhakikisha wanapika vyakula katika mazingira ya usafi ili kuepuka maradhi mbalimbali hususan magonjwa ya Milipuko.


Naye Afisa Ustawi wa Jamii bi Leah Mayagi  amewataka wakina mama kuzingatia kanuni za unyonyeshaji kwa kuhakikisha mtoto ananyonya kwa miezi sita bila kupewa chakula cha ziada kwani maziwa ya mama ni lishe iliyokamilika.


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa