• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

JAMII YAASWA KUENDELEA KUPANDA MITI NA KUTUNZA MAZINGIRA

Posted on: April 14th, 2024

Katibu Tawala Wilaya ya Kilosa  Bi. Salome Mkinga ameitaka jamii kuendelea kutambua umuhimu wa ustawi wa mazingira kwa kuhakikisha kila mwanajamii anashiriki kikamilifu katika kutunza mazingira na kuyalinda kwa kushiriki katika mazoezi yote ya upandaji miti na utunzaji mazingira ikiwa ni katika kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutunza na kustawisha mazingira.


Mkinga ameyasema hayo Aprili 13. 2024 wakati akiongoza kampeni ya upandaji miti katika shule ya Msingi Dumila Juu ambapo amesema Serikali imekuwa ikifanya jitihada kubwa katika kutunza mazingira na kuhakikisha nchi inakuwa katika ustawi bora hususani upande wa mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ambapo ametaka kila mmoja kushiriki katika utunzaji wa miti inayopandwa katika maeneo mbalimbali huku akitoa rai kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru kwa kuzingatia na kuifanyia kazi kauli mbiu  ya Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2024 isemayo ’’Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu‘‘ ambapo Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kupokelewa  na kukimbizwa wilayani Kilosa ifikapo tarehe 22/04/2024.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Ndg. Michael J. Gwimile amesema zoezi la upandaji miti ni la msingi ambapo maelekezo ya Serikali kwa sasa ni uboreshaji mazingira ili kuweza kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi ambapo kwa sasa hali ya mvuai ni nyingi, hivyo ni vema watu wakazingatia kutokata miti na kufyeka mapori hovyo na badala yake kila mmoja aweke kipaumbele katika  kuhamasisha upandaji miti jambo litakalosaidia kuwa na mazingira bora.

Mh. Deoglas Mwigumila ambaye ni diwani wa kata ya Dumila ameushukuru uongozi wa Wilaya ya Kilosa kwa kufanya kampeni ya upandaji miti katika kata yake ambapo amesema wamejipanga kuwa mabalozi wazuri wa upandaji miti na kutunza mazingira huku akimshurkuru Mheshimiwa Rais kwa ajili ya fedha zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya Misungi ambayo inatarajiwa kufunguliwa na Mwenge wa Uhuru na kwamba shule hiyo ni msaada mkubwa kwa wanafunzi kusoma kwa nafasi.

Naye Kaimu Mhifadhi Misitu TFS Bi.Hilda Mwalongo amesema kwa mwaka 2023/24 Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira ilitoa Malengo ya Kitaifa kila Wilaya kupanda miti laki moja na nusu (1,500,000) ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ikiwa ni kampeni shirikishi ambapo mpaka sasa wilaya ya Kilosa jumla ya miche ya miti 1,389,466 kati ya 1,500,000 imepandwa sawa na 92.63% huku zoezi likiwa ni endelevu.

Aidha amesema ipo mikakati ili kufanikisha lengo ikiwemo kutoa Elimu ya Mazingira kwa jamii, Kuanzisha klabu za Mazingira mashuleni, Kushirikisha jamii kwenye masuala ya Mazingira, Kuunda, kusimamia na kuboresha kamati za maliasili zilizopo, kuendelea kutoa elimu ya uchomaji moto na kutunza vyanzo vya maji, kuendelea kushirikiana na Wadau wa Mazingira kwenye masuala ya kimazingira, kuhamasisha Serikali za vijiji kusimamia kikamilifu miti iliyopandwa na Misitu iliyopo, Kuweka ulinzi kwenye vyanzo vya maji kwa kushirikiana na mamlaka za maji na bonde sambamba na kuendelea kutenga bajeti kwa ajili ya upatikanaji wa  vitendea kazi katika vitalu vya miche.  


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa