• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

JAMII YAASWA KUPIMWA AFYA ZAO

Posted on: May 19th, 2020

 Mwenyekiti wa Kamati Shirikishi ya Kudhibiti Ukimwi Wilaya ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mh. Hassan Kambenga amevitaka vikundi mbalimbali vya watu wenye maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutambua mchango unaotolewa na Halmashauri kwa kuhakikisha vinahamasisha jamii kupima afya zao.

Kambenga ametoa rai hiyo Mei 19 mwaka huu wakati alipokuwa akifungua kikao kilichokuwa kinalenga kufanya uchaguzi wa viongozi wa baraza la watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI wilayani Kilosa ambapo amesema zipo faida mbalimbali za jamii kupima na kujua afya zao ikiwemo kujua tatizo na kupata tiba mapema ambapo amewataka washiriki wa kikao hicho kuendelea kuhamasisha jamii kupima afya mara kwa mara na kuchukua hatua stahiki.

Kambenga amesema kwa upande wa vikundi vya watu wenye VVU ni rahisi kupata sapoti toka serikalini na Halmashauri kiujumla sambamba na kupata misaada ya kiuchumi ambapo amesema vikundi hivyo vinahitaji kuwa hai badala ya kudorora ambapo kwa sasa vikundi vilivyo hai wilayani Kilosa vipo 10 kati ya vikundi 24 vinavyotambulika jambo linalopelekea hali ya utendaji kazi katika kuvihudumia vikundi hivyo kuwa ngumu kutokana na kudorora kwa vikundi hivyo.

Akizungumzia upande wa mradi wa Hebu Tuyajenge Kambenga amesema mradi huo unatarajiwa kufanya kazi katika kata tano zenye hali ya juu ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI ambapo upande wa viongozi watakaochaguliwa amewataka kuiga mfano mzuri wa viongozi waliopita lakini pia kuhamasisha vikundi vilivyodorora kuinuka upya, kuhamasisha jamii kupima afya lakini kusimamia uanzishwaji wa vikundi vipya ili viweze kupata sapoti kutoka Halmashauri.

Akizungumzia uwepo wa mradi wa Hebu Tuyajenge Afisa Ufuatiliaji na Tathmini Bi. Sophia Liundi amesema mradi huo ni mradi wa miaka mitano ambao unaofadhiliwa na Shirika la Watu wa Marekani USAID ukiwa na lengo la kuongeza mapambano ya kupunguza maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI nchini Tanzania ambapo wilayani Kilosa unatarajiwa kufanya kazi katika kata tano za Rudewa, Dumila, Mikumi, Kasiki na Kidodi.

Naye Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Rwegerera Katabaro pamoja na Mratibu wa UKIMWI Wilaya Merrisiana Temu kwa pamoja wameushukuru uongozi uliopita kwa kazi kubwa waliyofanya kwa kipindi chao cha uongozi huku wakiwataka viongozi wateule kufanya kazi kwa bidii na kwa moyo ili kuhakikisha vikundi hivyo vinakuwa imara kwani Halmashauri ipo kwa ajili ya kuwasaidia na kuwapa sapoti ili waweze kusonga mbele.

Katika uchaguzi huo uliochagua viongozi kwa ngazi mbalimbali umefanikiwa kumchagua Rashid Namtuka kwa nafasi ya Mwenyekiti, Makamu Mweneykiti akiwa ni Mariana Lucas, Zuhura akiwa Katibu, Mweka hazina Rehema Seif na viongozi wengineo ambao watakuwa wakishiriki katika vikao vya Kamati Shirikishi ya Kudhibiti Ukimwi Wilaya.

Tangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA WAHE. MADIWANI May 22, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WAUGUZI WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAHALI PA KAZI

    May 30, 2025
  • WAHE. MADIWANI WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 30, 2025
  • KILOSA YAJIPANGA KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

    May 28, 2025
  • VITENGO VYA HABARI SERIKALINI VIIMARISHWE KWA KUFANYA MAWASILIANO YA KIMKAKATI

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa