• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

JAMII YAENDELEA KUHAMASISHWA KUPATA CHANJO YA UVIKO 19 ILIKUWA SALAMA

Posted on: October 6th, 2021

Katika kuendesha kampeni maalum ya utoaji elimu na chanjo ya UVIKO 19 ndani ya  siku 14 ya nyumba kwa nyumba, mtaa kwa mtaa inayoendelea nchi nzima kuanzia Oktoba 1 hadi 14 mwaka huu Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mh. Majid Mwanga ametoa rai kwa wananchi kujikita zaidi kwa kuwasikiliza wataalam wa afya ili kupata elimu ya pamoja juu ya UVIKO 19 badala la kujikita zaidi katika kutafiti kupitia mitandao ya kijamii.

Mwanga ametoa rai hiyo Oktoba 6 mwaka huu wakati wa kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi ya Chanjo ya UVIKO 19 ambapo ameitaka kamati hiyo kupata elimu ya pamoja juu ya ugonjwa huo ambapo ametaka kufuatwa kwa masharti na ushauri unaotolewa na wataalam ili kuwa msaada kwa jamii isiyo na uelewa juu ya UVIKO 19.

Aidha ameitaka kamati hiyo kuwa mabalozi wa kutoa elimu kwa jamii inayowazunguka ili kuisaidia jamii kila mmoja katika eneo lake kwani chanjo ni salama na kwamba suala la upotoshaji katika jamii halikosekani, hivyo kila mmoja awe mfano katika kuhamasisha wale ambao hawajapata chanjo ili waweze kupata chanjo ili kuwa salama kiafya.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Kisena Mabuba amesema chanjo ya UVIKO 19 ni muhimu kwa kila mmoja kwani kati ya changamoto za maradhi zilizopo mojawapo ni UVIKO 19 hivyo Serikali imejipanga kuhakikisha wananchi wake wanapata chanjo kwa kuhakikisha elimu ya umuhimu wa chanjo inatolewa  kwa wananchi ikiwa imeambatana na shughuli za uchanjaji hivyo kupitia kamati hiyo anaamini hamasa itafanyika ya kutosha ili kutoa elimu.

Pamoja na hayo amesema Halmashauri imejipanga vizuri kuhakikisha jamii inafikiwa na kupata elimu pamoja na chanjo huku akisema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu amekuwa mhamasishaji mkuu kwa jamii kupata chanjo kwani chanjo ni salama hivyo Halmshauri iko tayari kufika maeneo yote ili kutoa elimu na chanjo lengo ikiwa ni kupunguza maambukizi. 

Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Dkt. George Kasibante amesema kwa sasa vituo vyote vinatoa huduma ya chanjo ya korona tofauti na awali ilipoana huduma ya utoaji chanjo ilikuwa ikitolewa katika vituo vitatu tu na kwamba lengo la utoaji chanjo dhidi ya UVIKO-19 ni kupambana na ugonjwa huo unaozuilika  kwa chanjo, Kupunguza vifo vitokanavyo na ugonjwa wa Korona, Kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo huku akisema kuwa unafanyika uhamasishaji kwa lengo la kuhakikisha kuwa jamii inahamasika na kuelewa umuhimu wa chanjo ya UVIKO-19 ili kupata ushirikiano na kuchanja.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa