• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

JAMII YAHAMASISHWA KUTUMIA KINGA TIBA ILI KUKABILIANA NA MAGONJWA MBALIMBALI

Posted on: August 27th, 2019

Mratibu magonjwa ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele Wilaya Bi.Rose Nguruwe amebainisha kuwa magonjwa ya trakoma, usubi, kichocho, minyoo, matende na mabusha ni magonjwa ambayo yanadhibitiwa  na mpango wa Taifa kwa kutolewa madawa katika maeneo mbalimbali hususani mashuleni kwenye kaya kama kinga lakini pia hutolewa kwa wagonjwa ambao tayari wameshaathirika na magonjwa hayo..

Akifafanua magonjwa hayo Agosti 27 mwaka huu katika kikao uhamasishaji kilichoshirikisha viongozi wa dini, viongozi wa siasa na wakuu wa idara na vitengo Rose amesema kuwa upande wa ugonjwa wa kichocho huenezwa kupitia binadamu kwa kueneza vimelea vya ugonjwa kwa njia ya kujisaidia katika vyanzo vya maji ambapo vimelea hivyo huingia kwenye konokono kwenye maji yaliyotuama  ambapo husababisha damu kutoka kwenye mkojo na kinyesi na baadae inaweza kusababisha saratani ya tumbo, kibofu cha mkojo na ini.

Kwa upande wa minyoo ya tumbo huathiri zaidi jamii maskini ambapo huambukizwa kwa kula mayai ya minyoo na namna ya kujikinga ni kwa kutumia dawa za minyoo na kuongeza kiwango cha usafi.

Nguruwe amesema mabusha na matende husababishwa na minyoo midogo inayoathiri mfumo wa maji na huenezwa na mbu wa aina zote kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine ambapo amesema kuwa matibabu yanatolewa hivyo mgonjwa afike hospitali kupata matibabu,na ameshauri matumizi ya vyandarua muda wote sambamba na kutunza mazingira ili kuepeusha mazalia ya mbu.

Akielezea usubi ni nini, amesema ni ugonjwa unaosababishwa na minyoo ya filaria aina ya Onchecerca Volvulus na kusambazwa na inzi weusi wadogo wa kike wajulikanao kama Simulium ambao huzaliana kwa wingi kwenye maeneo yenye vijito/mito yenye maji yanayotiririka kwa kasi.

Licha ya uwepo wa magonjwa hayo Muuguzi Mkuu Wilaya Bi Mwanaisha Chitanda amesema kuwa magonjwa hayo yanatibika na kwamba ipo haja ya jamii kutumia kinga tiba na kwamba dawa hizo ni salama na hazina matatizo yoyote hivyo ni vema jamii ikahamasishwa kutumia kinga hizi ili iweze kumeza dawa kwa wingi ambapo dawa hizo hutolewa katika kaya , vibanda Maalum, makundi maalum mfano walemavu na kwamba katika suala zima la utoaji dawa huzingatia uzito na umri ambapo huanza kutolewa kwa watoto kuanzia miaka mitano.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa