• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

JAMII YAPASWA KUFAHAMU UMUHIMU WA MALEZI NA MAKUZI YA MTOTO

Posted on: December 24th, 2020

Malezi kwa makuzi ya mtoto yana faida kwa maisha ya baadaye ya mtoto hasa katika kumuimarisha kiuchumi na kuboresha maisha yake ikiwemo kuwa na uwezo wa kufikiri na kuchanganua mambo, viungo kufanya kazi vizuri mfano macho na mikono, kusikia na uwezo wa kuongea kiufasaha, pia mtoto kukabiliana na changamoto za ukuaji zinazochangia kusababisha udumavu na kuwa na uboreshaji wa maisha ya mtoto ya baadae kiafya, kielimu, kijamii na kiuchumi.


Hayo yamebainishwa Disemba 23 mwaka huu na Afisa Lishe Wilaya Zaina Kibona wakati wa kikao cha kamati ya lishe na watendaji wa kata ambapo amesema kuwa huduma za makuzi ya awali ya mtoto zinasaidia  watoto wenye utapiamlo mkali kuongezeka uzito zaidi na kurudia katika hali ya kawaida kwa haraka zaidi ukilingalisha na wanapopata chakula dawa peke yake ambapo pia inamsaidia mtoto kuwa na uwezo wa kujiamini katika kujieleza, kufanya vizuri katika masomo, kufanya maamuzi sahihi na kukabiliana na changamoto mbalimbali.

Akieleza suala zima la ukuaji wa mtoto kiakili, kijamii, kihisia na kimaadili amesema inasaidia mtoto kuongezeka kwa ufahamu, uwezo wa kufikiri, kutafakari na kutatua matatizo kulingana na umri wake kwani mtoto huanza kujifunza juu ya mazingira anayoishi kwa kutumia milango ya fahamu (kuona, kusikia, kunusa, kuonja na kugusa) huku upande wa kihisia inamsaidia kumwezesha mtoto kuelewa hisia zake na kujifunza namna ya kuzidhibiti.

Kibona amesema mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika na msongo wa mawazo ya mama hivyo ipo haja ya wazazi kuwa makini kwa kila wanachokifanya hususani katika kipindi cha ujauzito ikiwemo kuzungumza na mtoto wao tangu akiwa tumboni lakini pia kuzingatia mavazi ya mama mjamzito ambapo anapaswa kuvaa mavazi yatakayomruhusu mtoto kucheza vizuri (yasiyobana), kupumzika na kusaidiwa kazi nzito na wanafamilia wengine  sambamba na kuacha vitendo vya ukatili kwa mama mjamzito mfano kupigwa, maneno makali n.k. ambavyo haviruhusiwi hata kidogo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa