• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

JAMII YASHAURIWA KUENDELEA KUTUNZA MAZINGIRA

Posted on: May 18th, 2023

Wito umetolewa kwa viongozi mbalimbali na wananchi kiujumla kuendelea kuiishi kaulimbiu ya mbio za Mwenge wa Uhuru katika maeneo yao kwa kuhakikisha mazingira yanatunzwa ipaswavyo kwa maslahi mapana ya uhai wa viumbe hai pamoja na uchumi wa taifa kwani kumekuwepo na mabadiliko ya tabianchi  ambao umesababishwa kwa kiasi kikubwa na shughuli za kibinadamu.

Hayo yamebainishwa Mei 17 mwaka huu na mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mh.Wilfred Sumari katika kikao cha baraza la Madiwani ambapo amesema kuwa kupitia mabadiliko ya tabianchi ipo haja ya wilaya kuendelea kuiishi kauli mbiu hiyo kwa kila mmoja kwa kutunza mazingira kwani vyanzo vya maji vimeendelea kukauka lakini pia kumekuwepo na hulka ya baadhi ya watu kuchafua vyanzo vya maji jambo ambalo si sahihi.,

Akizungumzia suala la mapato amesema ipo haja ya halmashauri kuendelea kubuni vyanzo vya mapato vyenye uhakika ili kuinua mapato ya halmashauri kwa kuweka mikakati madhubuti ikiwemo kujenga stendi za mabasi na maegesho ya malori mikumi na dumila,Sambamba na hayo Mh Sumari amewataka watendaji wa idara mbalimbali za Halmashauri kubuni vyanzo vipya vya mapato vya uwakika ambavyo vitakuwa mali ya kilosa kwa ajili ya kuongeza ukusanyaji wa mapato yatakayosaidia kuboresha huduma na shughuli mbalimbali za kuwaletea maendeleo wananchi wa  Wilaya ya Kilosa

Pamoja na hayo ameishukuru uongozi wa Rais wa awamu ya sita Mh Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa shilingi Bilioni 2,025,800 kupitia mradi wa kuboresha Elimu ya Awali na Msingi Tanzania (BOOST)  ambapo fedha hizo zitasaidia kujenga shule, vyumba vya madarasa na vyoo hivyo kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Kisena Mabuba amewaomba madiwani wa kata kushiriki kikamilifu katika usimamizi na utekelezaji wa mradi wa BOOST ambapo ametaka kuwepo na hali ya uhakiki na kijiridhisha kwa bei za vifaa na uletwaji wa bidhaa  za ujenzi katika maeneo yatakapofanyika miradi ya BOOST jambo litakalosaida kutokiukwa kwa utekelezaji wa miradi hiyo lakini pia utapelekea  miradi hiyo kufanyika kwa ubora wa thamani ya fedha.

Aidha ametoa rai ya usimamizi wa miradi mingine inayoendelea katika kata mbalimbali ikiwemo miradi katika sekta ya elimu, afya na mingineyo kuwe na usimamizi wa matumizi ya fedha ambapo zinapaswa kutumika ipasavyo kwa kufuata taratibu ili kujiepusha na suala la uwepo wa fedha za bakaa lakini pia amesisitiza suala la ushirikiano na umoja katika kuiendesha halmashauri hususani katika suala la ukusanyaji wa mapato katika vyanzo mbalimbali.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WAKUMBUSHWA KUZINGATIA MAADILI

    June 05, 2023
  • Vikundi vilivyopata mikopo vyatakiwa kufanya marejesho kwa wakati

    June 02, 2023
  • Vikundi vilivyopata mikopo vyatakiwa kurejesha kwa wakati

    June 02, 2023
  • Shaka aahidi kushirikisha wananchi utatuzi wa changamoto

    May 31, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa